Posts

Showing posts from June, 2025

MASUNGA MASELE AJITOSA UBUNGE JIMBO LA SEGEREA

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Kada wa Chama Cha Mapinduzi Masele Masunga, amechukua fomu kugombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Segerea wilaya ya Ilala mkoa Dar es Salaam.  Masunga Masele amekabidhiwa fomu hiyo Juni 30,2025 na Katibu CCM Wilaya ya Ilala Sylvester Yared ili aweze kupata ridhaa ya kuteuliwa aongoze wananchi wa Segerea.  Akizungumza ccm Wilaya ya Ilala Masunga Masele amesema kuwa amepata msukumo kutoka kwa Wananchi wa Jimbo la Segerea kumtaka agombea kwa madai kuwa bado kuna mambo yanatakiwa kuongezewa nguvu ili kuwaletea maendeleo wananchi. Alisema kuna matatizo mbalimbali yanayoilikabili Jimbo hilo ikiwemo ukosefu wa ajira kwa Vijana,huduma za afya, Elimu na ubovu wa baadhi ya miundombinu ya barabara .

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image

KASI YA UTEKELEZAJI WA MRADI WA UMEME JUA KISHAPU, WAMKOSHA BALOZI WA UFARANSA

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Balozi wa Ufaransa Nchini Tanzania Bi. Anne Sophie Ave ametembelea na kukagua Mradi wa kuzalisha umeme wa Jua (solar) uliopo Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga na kujionea kasi kubwa ya maendeleo ya utekelezaji wa Mradi huo ambao mpaka sasa umefikia asilimia 67. Akizungumza katika ziara hiyo Juni 27,2025 Balozi amesema kuwa dhumuni la ziara hiyo ni kuona utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Tanzania ambayo inafadhiliwa na umoja wa Nchi za ulaya ikiwemo Ufaransa na Shirika la Maendeleo la Ufaransa “Sababu kubwa ya mimi kuja hapa, ni kutaka kujionea miradi ya maendeleo ambayo Umoja wa Nchi za Ulaya na Shirika la maendeleo la Ufaransa inaifadhili, ikiwemo mradi huu wa kuzalisha umeme wa jua hapa Kishapu, nimeona tija ya mradi huu kwa wananchi lakini pia nimeona thamani ya pesa ambayo tumeitoa, kazi ni nzuri na watendaji kazi hapa wanafanyakazi kwa bidii na kujitoa sana, niwaombe waendelee kujitoa ili mradi huu ukamilike kwa wakati na watanzania wapa...

WATAALAM SADC WAKUTANA ZIMBABWE KUJADILI SEKTA YA NISHATI NA MAJI

Image
📌 *Miundombinu ya usafirishaji umeme kikanda kujadiliwa* 📌 *Nishati Safi ya kupikia kupewa kipaumbele* 📌 *Mkakati mahsusi wa kuongeza watumiaji wa umeme Afrika (M300) kuwa moja ya Ajenda* 📌 *Maendeleo ya Sekta ndogo ya Mafuta na Gesi pamoja na umeme vijijini kujadiliwa* Wataalam wa Wizara ya Nishati pamoja na taasisi zake leo wameshiriki katika Mkutano wa ngazi ya Makatibu Wakuu na Watalaam wanaoshughulikia masuala ya Nishati na Maji unaofanyika katika Jiji la Harare nchini Zimbabwe.  Mkutano huo wa awali ni sehemu ya maandalizi kuelekea katika Mkutano wa pamoja wa Kamati ya Mawaziri wanaoshughulikia masuala ya Nishati na Maji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).  Mkutano huo pamoja na kujadili masuala ya Nishati na Maji, umekuwa ni fursa pia kwa Tanzania kuendeleza diplomasia ya kiuchumi pamoja na kuwasilisha mafanikio ya nchi katika kuboresha huduma za nishati vijijini kupitia miradi inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijjni (REA).  Aidha, Mkutano...

BALOZI CHANA AWAVISHA VYEO MANAIBU KAMISHNA WAWILI NA KUSHUHUDIA UVISHWAJI VYEO WA MAKAMISHNA WASAIDIZI WAANDAMIZI WATANO WA NCAA.

Image
Kassim Nyaki, NCAA Arusha. Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) amewavisha cheo manaibu kamishna wawili na kushuhudia uvishwaji vyeo kwa makamishna wasaidizi waandamizi watano waliovishwa vyeo na mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi NCAA Jenerali Venance Mabeyo (Mstaafu) Waliovishwa Cheo na Mhe. Waziri ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Joas John Makwati aliyepandishwa cheo kuwa Naibu Kamishna wa Uhifadhi anayesimamia Uhifadhi, utalii na Maendeleo ya Jamii na Naibu Kamishna wa Uhifadhi Aidan Paul Makalla anayesimamia Huduma za Shirika NCAA. Kwa upande wa makamishna waliovishwa vyeo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi NCAA Jenerali Venance Mabeyo (mstaafu) ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia idara ya Mipango na uwekezaji, Gasper Stanley Lyimo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Paul Geofrey Shaidi anayesimamia Kitengo cha huduma za Sheria, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Charles Marwa Wangwe anayesimamia Idara ya Uhasibu n...

RAIS MWINYI AIZAWADIA MILIONI 100 KLABU YA YANGA.

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi ameizawadia Klabu ya Yanga SC shilingi milioni 100, kwa kutambua ushindi na mafanikio makubwa waliopata katika msimu wa mwaka 2024/2025. Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 30 Juni 2025 alipokutana na viongozi pamoja na wachezaji wa Yanga waliofika Ikulu kwa ajili ya kumkabidhi makombe matano ya michuano mbalimbali waliyoyatwaa msimu huu. Akizungumza nao, Rais Dkt. Mwinyi amepongeza mafanikio hayo makubwa yaliyopatikana na klabu hiyo kongwe, akieleza kuwa yanajenga heshima na historia muhimu katika tasnia ya michezo nchini. Aidha, ameishukuru Yanga kwa kuendelea kuitangaza Zanzibar ndani na nje ya nchi kupitia kampeni ya Visit Zanzibar, huku akieleza kuwa hatua ya klabu hiyo kucheza baadhi ya michezo yake Zanzibar kunachangia kukuza uchumi na sekta ya utalii kutokana na kuongezeka kwa idadi ya wageni na wananchi kunufaika na fursa mbalimbali. Halikadhalika, Rais ...

DKT. BITEKO ASEMA NISHATI ITAKAYOZALISHWA NA NYUKLIA KUJUMUISHWA KWENYE GRIDI YA TAIFA

Image
  Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  📌 Asema ni Nishati yenye unafuu wa gharama kulinganisha na vyanzo vingine vya nishati, pia isiyochafuzi kwa mazingira. 📌 Asisitiza nyuklia kwa ajili ya kuzalisha umeme ni salama, awatoa hofu jamii kuhusiana na matumizi yake 📌 Akazia kuhusiana na matumizi ya Vinu vidogo vinavyotumia teknolojia ya kisasa ya Small Module na Micro Reactors  📌 Nyuklia yatajwa kuleta mapinduzi ya kweli ya uchumi na viwanda Afrika 📌 Rais Samia adhamiria Tanzania kuzalisha umeme wa nyuklia Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa Tanzania inatarajia kuzalisha umeme unaotokana na nyuklia utakaojumuishwa katika Gridi ya Taifa ili kukabiliana na ongezeko la mahitaji ya umeme yanayotokana na ongezeko la viwanda. Dkt. Biteko amesema hayo Juni 30, 2025 Kigali nchini Rwanda wakati akihutubia katika Mkutano kuhusu masuala ya Nyuklia Afrika. “Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...

DKT KAZUNGU AKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN, WAAHIDI KUWEKEZA KWENYE MIRADI YA UMEME

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  📌Pia kuwekeza kwenye miundombinu ya usafirishaji umeme nchini 📌Waialika Tanzania kushiriki mkutano wa Tisa wa maendeleo kati ya Japan na Afrika 📌 Waupongeza mpango mahsusi wa Nishati wa Taifa kuwa bora na wa mfano kwa nchi za Afrika Naibu katibu Mkuu Wizara ya Nishati, anayeshughulikia umeme na nishati jadidifu Dkt Khatibu Kazungu, leo amekutana na kuzungumza na ujumbe wa wawekezaji kutoka nchini Japan kupitia kampuni ya Toyota Tshusho Cooperation, uliolenga kufanya mazungumzo kuhusu uwekezaji wa miradi mbalimbali kwenye sekta ya umeme hususan umeme wa jua, upepo na njia za kusafirisha umeme pamoja na ujenzi wa vituo vya kupoza umeme chini ya mpango mahsusi wa Nishati wa Taifa ujulikanao kama Energy Compact.  Kupitia serikali ya Japan chini ya Japan International Banking Corporation, Japan imeonesha nia yake ya kuwekeza kwenye maeneo hayo na kwa sasa wapo kwenye mazungumzo na Serikali ya Tanzania ili kuainisha maeneo hayo ya uwekezaji.  ...

PETER MASHILI KUVAANA NA BASHE JIMBO LA NZEGA MJINI

Image
  Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya MASHILI COMPANY LIMITED ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mradi wa Uchenjuaji Dhahabu wa (Matinje Mining, Msilale Mining na Igurubi Mining) Ndg Peter Andrea Mashili ametangaza nia ya Kugombea Ubunge wa Jimbo la Nzega Mjini akiahidi kumg'oa Mbunge aliyepo Mhe Hussein Bashe ambaye ni Waziri wa Kilimo kwa madai kwamba anastahili kupumzika baada ya kuwatumikia wananchi katika kipindi cha miaka kumi. Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ndani ya Chama Cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Nzega, Peter Mashili amesema kuwa ameamua Kugombea Ubunge kwa sababu wananchi wa Nzega wanahitaji nguvu na kasi Mpya ili kuendeleza utekelezaji wa ilani ya CCM katika kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka 2025-2030. Amesema akiteuliwa na Chama Cha Mapinduzi kwenye mchakato wa kura za maoni na baadaye akiteuliwa kuwa mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM Jimbo la Nzega Mjini atajikita zaidi katika ushirikishwaji wa wananchi...

CLARA BUNDU AOMBA RIDHAA KUGOMBEA UDIWANI VITI MAALUM KATA YA BUNJU

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU   MJUMBE wa Jumuiya ya Wanakwe wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Tawi la Boko Clara Bundu amechukua fomu ya kutia nia kuwania udiwani wa Viti Maalum Kata ya Bunju, Tegeta Halmashauri ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam. Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 29, baada ya kukabidhiwa fomu hiyo ameomba ridhaa ya Chama cha Mapinduzi kumpatia na fasi ili kuwatumikia wananchi. Amesema hadi leo yeye ni mwanamke pekee kwa Kata ya Bunju aliyejitokeza kuchukua fumo kumba ridhaa hiyo. Mgombea huyo amechukua fomu katika ofisi za Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kinondoni, ambapo amekabidhiwa na Katibu wa UWT wa Wilaya hiyo, Haziati Juma.

ANNETH MASEGESE ATIA NIA KUCHUKUA FOMU YA UDIWANI VITI MAALUM KATA YA MSASANI

Image
  Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  MJUMBE wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wanawake wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Tawi la Chama Oyster Bay, wilayani Kinondoni mkoani Dar es Salaam, Aneth Masegese amechukua fumu ya kuomba ridhaa ya kugombea nafasi ya Udiwani Viti Maalum Kata ya Msasani. Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhiwa fomu hiyo, Masegese amesema kuwa amefanya hivyo ili kutia hamasa kwa wanawake wengine kujitokeza na kuchukua fomu kuomba kugombea nafasi mbalimbali. "Nmeona ninafaa na ninaweza ndiyo maana nimeamua kuchukua hii fomu kama chama changu cha mapinduzi pia kitanipitisha itakuwa ni jambo jema na heshima kwangu na kwa wanawake wanaojiamini na kuthubutu," amesema Masegese. Mgombea huyo amechukua fomu katika ofisi za Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kinondoni, ambapo amekabidhiwa na Katibu wa UWT wa Wilaya hiyo, Haziati Juma.

COMORO MWENDA AJITOSA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA KAWE

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU   MBOBEZI wa Kazi katika Utumishi wa Umma Kimataifa, Comoro Mwenda (kushoto), amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya Chama cha Mapinduzi kumpitisha kugombea Ubunge Jimbo la Kawe.  Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 29, 2025 mkoani Dar es Salaam baada ya kukabidhiwa fomu hiyo, Mwenda amesema anauzoefu mkubwa katika kufanya kazi na mashirika makubwa ya kimataifa. Hivyo amesema kuwa hajachukua fomu kama fasheni bali anania thabiti ya kuwatumikia wananchi endapo atapatiwa ridhaa ya chama chake cha CCM. Mwenda, amekabidhiwa fomu na Katibu wa Jumuiya ya Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Amos Richard.

GRACE MUSHI AJITOSA KUWANIA UDIWANI VITI MAALUM MABWEPANDE

Image
  Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Mweneyekiti wa Jumuiya ya Wanakwe wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Shina namba 13 Bunju B Mkoa wa Dar es Salaam Grace Mushi amechukua fomu ya kutia nia kuwania udiwani wa Viti Maalum Kata ya Mabwepande Halamshauri ya Kinondoni. Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 29, 2025 baada ya kukabidhiwa fomu hiyo Mushi amesema lengo ni kutaka kupambania maendeleo ya wananake. Hivyo ameomba ridhaa ya Chama cha Mapinduzi kumpatia na fasi ili kuwatumikia. Mgombea huyo amechukua fomu katika ofisi za Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kinondoni, ambapo amekabidhiwa na Katibu wa UWT wa Wilaya hiyo, Haziati Juma.

DKT. BITEKO AWASILI RWANDA KUSHIRIKI MKUTANO WA NYUKLIA AFRIKA

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt Doto Biteko Juni 29, 2025 amewasili Kigali nchini Rwanda kwa ajili ya kushiriki katika Mkutano unaohusu masuala ya nyuklia Afrika. Katika Mkutano huo unaotarajiwa kuanza Juni 30 hadi Julai 1, 2025 nchini humo unajumuisha wadau wa nishati kutoka ndani na nje ya Afrika wenye lengo la kuharakisha matumizi ya nyuklia kwa kutumia teknolojia ya kisasa ili kuleta mabadiliko ya nishati Afrika. Pamoja na ushiriki wake katika Mkutano huo Dkt. Biteko anatarajiwa kufungua mjadala wenye mada kuhusu nishati Afrika na utashi wa kisiasa. Aidha, katika Mkutano huo Dkt. Biteko ameambatana na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Cosato Chumi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba na Mkurugenzi wa Tume ya Mionzi ya Atomiki, Prof. Najat Mohamed.

MMILIKI MWANAMKE AONGOZA MAGEUZI YA UCHIMBAJI WA SHABA MPWAPWA

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Mpwapwa,Dodoma Mmiliki wa mgodi wa Ikombo Hill uliopo katika Kijiji cha Matonya, Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma, Bi. Doreen Kissia, ameibuka kuwa mfano wa kuigwa katika sekta ya uchimbaji wa madini ya shaba, akiwa mwanamke pekee anayeongoza mgodi unaotoa ajira kwa zaidi ya asilimia 98 ya wakazi wa vijiji vya Matonya na Kinusi. Bi. Doreen ameonesha uongozi bora na ubunifu kwa kufanikisha ujenzi wa barabara ya kilomita moja inayounganisha mgodi huo na barabara kuu, jambo lililorahisisha usafirishaji wa madini. Kwa sasa, mgodi huo unazalisha wastani wa tani 30 za madini ya shaba kwa mwezi. Akizungumza katika mahojiano maalum, Bi. Doreen ameiomba Serikali kusaidia kupeleka umeme katika mgodi wake ili kupunguza gharama kubwa za uendeshaji zinazotokana na matumizi ya jenereta. Kwa upande wake, Mhandisi Chacha Megewa wa Tume ya Madini, ametoa elimu kwa Bi. Doreen na wachimbaji wengine kuhusu umuhimu wa matumizi ya teknolojia ya uchenjuaji. Amebainisha kuwa c...

DKT. DOTO MASHAKA BITEKO ACHUKUA FOMU JIMBO LA BUKOMBE

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Mashaka Biteko aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Bukombe amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kutetea Ubunge katika Jimbo la Bukombe. Dkt. Biteko amechukua fomu hiyo na kuirejesha kwa Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Bukombe, Ndugu. Leonard Yesaya Mwakalukwa mapema leo Juni 29, 2025. Zoezi la uchukuaji fomu katika ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM) linaendelea nchi nzima ambapo watia nia tofauti wameendelea kujitokeza kwa ajili ya kuchukua fomu za Ubunge na Udiwani.

IDD AZZAN AJA KIVINGINE TENA JIMBO LA KINONDONI

Image
 Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azzan, akichukua fomu ya kugombea ubunge kwa mara nyingine kutoka kwa Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Kinondoni, Amos Richard, katika ofisi za chama hicho zilizopo Kinondoni. Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam Idd Azzan amechukua fomu ya kutia nia kugombea Ubunge Jimbo la Kinondoni, Dar es Salaam. Akizungumza leo Juni 29, 2025 baada ya kukabidhiwa fomu hiyo na Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama ch Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kinondoni Amos Richard katika Ofisi za CCM za Wilaya hiyo Azzan ameomba ridhaa Chama kimpitishe aweze kugombea nafasi hiyo. Azzan ambaye amewahi kuwa Mbunge wa Jimbo hilo, amesema alikuwa kimya Kwa muda Mrefu kwa sababu Jimbo lilikuwa tayari na Mbunge lakini Kwa sasa baada ya Miaka mitano sasa Jimbo liko wazi na Chama kimeweka Demokrasia ya kila mwenye nia kuchukua fomu.

MASOUD MAFTAH ACHUKUA TIKETI YA KUWANIA UBUNGE

Image
  Masoud Hassan Maftah akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhiwa fomu ya kutia nia kugombea Ubunge Jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi. NA MWANDISHI WETU JAMII HURU  KATIBU wa Diaspora Tanzania Masoud Hassan Maftah amechukua fomu ya kutia nia kugombea Ubunge wa Jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM). Akizungumza na waandishi habari baada ya kukabidhiwa fomu hiyo katika Ofisi za CCM Wilaya ya Kinondoni Maftah amesema ameamua kuchukua fomu Kwa sababu ni mkazi wa Kinondoni. "Mimi ninatia nia ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Kinondoni, nakiomba Chama kiweze kunipa fursa hii ili niweze kuwatumikia Wananchi," amesema Maftah. Kwamba anaamini kama atapatiwa ridhaa ya CCM kugombea nafasi hiyo atawatumikia vyema Wananchi wa Jimbo hio la akinondoni.

KASHASHA ALIGOMBEA JIMBO LA KAWE

  Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Katibu wa malezi,mazingira na afya wa chama cha Mapinduzi CCM,Eng Johnson Kashasha amechukua fomu ili kuomba ridhaa kwa chama hicho kumpitisha kama mgombea wa nafasi ya Ubunge Jimbo la Kawe. "nimechukua fomu hii kwa sababu mimi nina nia ya dhati kutoka moyoni kuhakikisha kwamba nawatumikia wananchi wa Jimbo Kawe" amesema. Aidha amesema kama chama kitamuona anafaaa ili kugombea katika jimbo hilo basi atakiwakilisha vyema. Makada mbalimbali wanaendelea kujitokeza kuchukua fomu kuwania Ubunge katika Jimbo hilo ambalo hapo awali lilikuwa likiongozwa na Askofu Josephat Gwajima.

RAIS SAMIA ATAJA MAFANIKIO SEKTA YA NISHATI 2020-2025

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  *📌Ni wakati akihitimisha shughuli za Bunge jijini Dodoma* *📌JNHPP, Umeme Vijijini, Umeme wa Gridi Kigoma na Katavi; Ni baadhi ya Vielelezo vya mafanikio* 📌 *Ataja miradi mikubwa ya usafirishaji umeme iliyokamilika* *📌Ataka TANESCO kuanza kuiangalia Nyukilia kama moja ya vyanzo vya kuzalisha umeme nchini.* Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameeleza kuwa Sekta ya Nishati imekuwa na mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka mitano.  Ameyasema hayo wakati akihitimisha shughuli za Bunge Jijini Dodoma tarehe 28 Juni 2025. "Mheshimiwa Spika kutokana na umuhimu wa Sekta ya Nishati kwa maendeleo ya nchi, Serikali imeimarisha upatikanaji wa nishati nchini ikiwemo kukamilisha mradi wa bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere (JNHPP)”. Amesema Mhe. Samia Ameongeza kuwa, mbali ya kukamirisha mradi wa Julius Nyerere pia Serikali imekamilisha upelekaji wa umeme katika Vijiji vyote 12,318 nchini. Ameongeza kuwa, msuku...

WACHIMBAJI WA SHABA WAASWA KUJIUNGA VIKUNDI KUNUFAIKA NA FURSA ZA MAENDELEO

Image
_Mpwapwa, Dodoma – Juni 28, 2025_ Wachimbaji wadogo wa madini ya shaba wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma wametakiwa kujiunga katika vikundi ili waweze kunufaika na fursa mbalimbali zinazotolewa na Mradi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), unaolenga kuwaendeleza wachimbaji wadogo wa madini ya kimkakati, ikiwemo shaba. Wito huo umetolewa na Mhandisi Chacha Megewa kutoka Tume ya Madini, wakati wa utoaji wa elimu kwa wachimbaji katika mgodi wa Minosphere, maarufu kama mgodi wa Majuto, uliopo Kijiji cha Kitati. Akizungumza na wachimbaji hao, Mhandisi Megewa amesema kuwa ni muhimu wachimbaji kuunda vikundi vya angalau watu watano, ili waweze kufikiwa kwa urahisi kupitia huduma kama mafunzo, uunganishwaji na taasisi za kifedha, pamoja na upatikanaji wa mikopo inayolenga kuongeza tija katika shughuli zao za uchimbaji. “Uchimbaji salama na wenye tija unahitaji ushirikiano na uratibu mzuri. Kupitia vikundi, wachimbaji watapata nafasi kubwa zaidi ya kunufaika na fursa za kitaifa na k...

GWIJI LA UCHUMI DKT KAHYOZA ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA MULEBA

Image
  Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Leo juni 28 , 2025 , Gwiji la uchumi nchini Dkt Bravius Kahyyoza amechukua fomu ya kugombea nafasi ya ubunge wa jimbo la Muleba Kusini mkoani Kagera.  Dkt Kayoza ni mmoja wa wataalamu wa uchumi nchini ambaye ameonesha dhamira yake ya kuwapigania wananchi wa Muleba Kusini kupitia uwakilishi wa muhimili wa bunge.

TFS YAWAKILISHA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA DUNIA KUHUSU MABADILIKO YA TABIANCHI

Image
Na Mwandishi Wetu – Bonn Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) umeiwakilisha Tanzania katika Mkutano wa 62 wa utekelezaji wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (SBI & SBSTA 62), uliofanyika jijini Bonn, Ujerumani, kuanzia tarehe 16 hadi 26 Juni, 2025. Mkutano huo wa kimataifa ulihusisha majadiliano ya kitaalamu kuhusu utekelezaji wa Itifaki ya Kyoto na Makubaliano ya Paris, ukilenga kuweka mikakati ya kupunguza uzalishaji wa gesi joto, kuhimili athari za mabadiliko ya tabianchi, na kuharakisha matumizi ya teknolojia rafiki kwa mazingira. Akizungumza kwa niaba ya TFS, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi kutoka TFS, SACC Dkt. Zainabu Bungwa, alisisitiza kuwa shughuli za uhifadhi wa misitu zinazofanywa na TFS zina nafasi muhimu katika juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi duniani.     “Mikakati ya TFS katika kuhifadhi na kuendeleza misitu ya asili na ya kupandwa ni nyenzo ya msingi katika kupunguza gesi joto, kuhifadhi vyanzo vya maji, na kuon...