KASHASHA ALIGOMBEA JIMBO LA KAWE
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU
Katibu wa malezi,mazingira na afya wa chama cha Mapinduzi CCM,Eng Johnson Kashasha amechukua fomu ili kuomba ridhaa kwa chama hicho kumpitisha kama mgombea wa nafasi ya Ubunge Jimbo la Kawe.
"nimechukua fomu hii kwa sababu mimi nina nia ya dhati kutoka moyoni kuhakikisha kwamba nawatumikia wananchi wa Jimbo Kawe" amesema.
Aidha amesema kama chama kitamuona anafaaa ili kugombea katika jimbo hilo basi atakiwakilisha vyema.
Makada mbalimbali wanaendelea kujitokeza kuchukua fomu kuwania Ubunge katika Jimbo hilo ambalo hapo awali lilikuwa likiongozwa na Askofu Josephat Gwajima.
Comments
Post a Comment