Posts

UBORESHAJI WA HUDUMA ZA WATEJA: MBUNGE BAGAMOYO AKABIDHI MAGARI KWA TANESCO

Image
Lengo ni kupunguza muda wa kushughulikia hitilafu na kuongeza ufanisi katika kuwahudumia wateja* Asema TANESCO imeimarika, imetoka katika kutengeneza hasara* 📍Bagamoyo, Pwani Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo, Mhe. Subira Mgalu leo Machi 03, 2026 amekabidhi magari mapya kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani kwa lengo la kuimarisha huduma kwa wateja na kuongeza ufanisi wa utendaji kazi katika kuwahudumia Wateja wilayani Bagamoyo. Akizungumza katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika Ofisi ya TANESCO Bagamoyo, Mhe. Mgalu amesema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme kwa wakati, kwa ubora na kwa uhakika zaidi. “Magari haya yatawezesha mafundi na wahandisi wa TANESCO kuwafikia wananchi kwa haraka pale panapotokea hitilafu au changamoto za umeme. Tunataka kuona muda wa kushughulikia matatizo unapungua na huduma inaboreshwa,” amesema Mhe. Mgalu. Amesisitiza kuwa, hivi sasa TANESCO imeimarika katika utoaji ...

NAIBU WAZIRI WA NISHATI SALOME MAKAMBA AKUTANA NA MKURUGENZI WA Go PLANT EMMANUEL LIKIDA KWA LENGO LA KUJADILI NAMNA YA KUSHIRIKIANA KATIKA MAANDALIZO YA MIJADALA

Image
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amekutana na Mkurugenzi wa Go Plant Tanzania Bw. Emmanuel Likida kwa lengo la kujadili namna ya kushirikiana katika maandalizi ya Mjadala (Debate) wa Clean Cooking Solutions utakaowahusisha wanafunzi wa shule za Sekondari katika Halmashauri za Mkoa wa Dodoma.  Katika kikao hicho, pande zote mbili zimejadili umuhimu wa kuwajengea vijana uelewa wa mapema kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia, athari za matumizi ya nishati zisizo safi kwa afya na mazingira, pamoja na fursa zilizopo katika ubunifu na ujasiriamali wa suluhisho za upishi safi. Mjadala huo unatarajiwa kuwa jukwaa la kielimu na kimkakati la kukuza uelewa, kuchochea fikra bunifu, na kuibua mabalozi vijana wa Nishati Safi katika jamii. Kikao hicho kimefanyika leo Machi 03,2026 katika Ofisi za Wizara ya Nishati zilizopo Mtumba, jijini Dodoma.

GEN'Z WAJIFUNZE AMANI ILIVYOSAIDIA USTAWI NA MAENDELEO YA NCHI- MANG'ATI

Image
  Vijana wa Kata ya Pugu, Wilayani Ilala Mkoani Dar Es Salaam wamehimizwa kusoma na kuijua Historia ya Tanzania na hatua kubwa za maendeleo zilizopigwa nchini, msingi ukitajwa kuwa amani, utulivu na usalama unaoshuhudiwa kote nchini. Kauli hiyo imetolewa na Mhe. Frank Mang'ati, Diwani wa Kata ya Pugu wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa amani kwa maendeleo na ustawi wa wananchi, akibainisha pia wajibu wake mkubwa katika kuhakikisha amani inaendelea kutawala katika eneo lake la kiungozi. "Mimi kama kama Kiongozi nawajibika kuhakikisha amani inakuwepo Pugu na huwezi kuongoza vyema kama amani hiyo hakuna. Amani ndio tunu ya Taifa letu na tunapaswa kuijali na kuienzi kwani amani na Utanzania wetu ndio inayotuunganisha." Amesisitiza Mhe. Mang'ati. "Sisi hatuna nchi nyingine zaidi ya Tanzania, tunao wajibu wa kuhakikisha nchi yetu inastawi na kushamiri katika amani. Wito wangu kwa Vijana almaarufu kama GenZ, Tujifunze tujue Taifa letu lilipotoka...

CRC YADAIWA BILIONI 4.7 NA TRA,MALI ZAKE ZIKISUBIRI KUPIGWA MNADA KUFIDIA DENI LA BENKI LA BILIONI 26.

Image
Na. Mwandishi wetu, Mamlaka ya mapato Tanzania, TRA inaidai zaidi ya shilingi bilioni 4.7 kama malimbikizo ya kodi kampuni ya Continental Reliable Clearling (CRC), fedha ambazo kampuni hiyo imezichepusha kwa matumizi binafsi badala ya kulipa kodi ya Watanzania  Hii inaibuka ikiwa ni siku chache zimepita baada ya kampuni hiyo ya CRC kugonga mwamba kuitumia Mahakama Kuu ya Tanzania kama kichaka cha kukwepa kulipa madeni, kwa mahakama hiyo kutupilia mbali maombi ya kampuni hiyo iliyoyapeleka dhidi ya benki za Equity Kenya na Tanzania na kuiagiza kampuni hiyo kulipa madeni waliyokopa na kuacha ujanja ujanja. Kufuatia uamuzi huo, tangazo la mnada wa mali za kampuni hiyo lililotolewa katika magazeti ya Mwananchi na The Citizen ya tarehe 19 mwezi wa pili kupitia kampuni ya udalali ya Adili Auction Mart Limited, lilithibitisha kuwa mali za CRC zinakwenda kuuzwa ili kufidia deni la benki linalofikia Shilingi bilioni 26. Hata hivyo, wakati harakati za mnada huo wa njia ya zabuni uliopangwa k...

JESHI LA POLISI LATOA TAMKO LA MWENYEKITI WA CCM ALIYEKUTWA AMEKUFA

Image
Kupitia mitandao ya kijamii kunasambazwa picha mjongeo akionekana mtu mmoja mwanaume ambaye anajinasibu kuhusika katika tukio la mauaji ya aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Tawi la Itumbi aitwaye Elia Richard Sambala, miaka 53, mkazi wa Itumbi Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya. Ukweli ni kwamba, Februari 11,2026 saa 7 mchana katika Kijiji cha Itumbi, Elia Richard Sambala, alikutwa shambani kwake akiwa amejeruhiwa kwa kukatwa na kitu chenye makali kichwani na watu wasiojulikana na alifariki dunia muda mfupi baada ya kufikishwa Hospitali ya Wilaya ya Chunya kwa matibabu. Kufuatia tukio hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, kupitia Askari wa kuchunguza matukio ya mauaji, walianza msako mkali na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili kuhusiana na tukio hilo na ufuatiliaji zaidi kwa wengine waliohusika unaendelea. Uchunguzi wa awali umebaini kuwa, chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa masilahi wa eneo la uchimbaji madini ya dhahabu ambapo mmoja wa wanafamilia hao alikodisha kwa wawekezaji raia wa Chin...

JESHI LA POLISI KUENDELEA KUWEKA JITIHADA ZA KUNUNUA MBWA WAPYA WA KISASA WENYE UWEZO WA KUBAINI,KUZUIA NA KUMDHOOFISHA MHALIFU.

Image
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillus Wambura, amesema Jeshi la Polisi litaendelea kuweka jitihada mbalimbali za kununua mbwa wapya wa kisasa na wenye uwezo ili kuboresha muonekano wa mbwa wa Polisi mwenye umbo lenye kumdhoofisha mhalifu. IGP Wambura, ameyasema hayo wakati wa Ufunguzi wa Kikao Kazi cha Wakuu wa Kikosi cha Mbwa na farasi wa Mikoa na Wataalam Waongoza Mbwa na Farasi kikao kilichofanyika jijini Dar es salaam Februari 9,2026 huku akiweka msisitizo kwenye eneo la utoaji wa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa kuwatumia Wanyama kazi katika kudhibiti uhalifu kwenye maeneo yao. Akizungumza na Watendaji hao IGP Wambura, amebainisha kuwa, Kikosi hicho kina umuhimu mkubwa kiusalama kwa kuwa Doria za mipakani na maeneo mengine muhimu hulazimika kutumia mbwa na farasi kwani ni rahisi kupenya kwenye maeneo ambayo gari haliwezi kupita kwa urahisi. Amesema, Jeshi la Polisi lina Mbwa na Farasi wanaofanya kazi katika bandari, viwanja vya ndege na mipakani kwa lengo la kuzuia biashara...

UPENDO NA MAELEWANO VYATAJWA KUWA MSINGI WA AMANI NCHINI

Image
Adam Seleman, Mkazi wa Msongora Jijini Dar Es Salaam amesema tafsiri halisi ya amani ni pamoja na kuelewana na kupendana miongoni mwa Watanzania, akihimiza upendo na maelewano kama msingi wa kudumisha amani na utulivu nchini. Bw. Selemani amebainisha hayo leo Jumamosi Februari 07, 2026 wakati akizungumza na mwandishi wetu wa habari kuhusu umuhimu wa amani kwa ustawi na maendeleo, akisema familia, Jamii na Nchi yoyote inahitaji amani na utulivu ili kuweza kutimiza majukumu na wajibu walionao. "Maana halisi ya amani ni ile hali ya mtu kuwa na uhuru wa kufanya jambo ambalo linaruhusiwa Kikatiba na pia amani tafsiri yake ni upendo, tukipendana ndio amani yenyewe kuanzia ndani ya nyumba. Nawaomba sana tuendelee kushikamana na kudumisha hiki tulichonacho kwani sisi nchi yetu ni kisiwa cha amani." Amesema Bw. Selemani.