Posts

WACHIMBAJI WADOGO DODOMA WAPATIWA MAFUNZO YA USALAMA, AFYA NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA MIGODINI

Image
_Mafunzo yanalenga kukuza uchimbaji salama, endelevu na wenye tija katika sekta ya madini ya shaba_ *Dodoma, Juni 27 2025* Wachimbaji wadogo kutoka migodi ya shaba iliyopo katika Mkoa wa Dodoma wamepatiwa mafunzo maalum kuhusu usalama mahali pa kazi, afya, utunzaji wa mazingira na usimamizi wa shughuli za uchimbaji.  Mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za kuimarisha uchimbaji salama na endelevu nchini. Mafunzo hayo yamewahusisha wachimbaji kutoka Mgodi wa Shengde uliopo Nala, Mgodi wa Hussein Pilly uliopo Tambi (Wilaya ya Mpwapwa) na Mgodi wa Canada uliopo Chamkoroma (Wilaya ya Kongwa) ambapo yamewezeshwa na Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP) kwa kushirikiana na Tume ya Madini. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mhandisi Chacha Megewa kutoka Tume ya Madini ameeleza kuwa ni muhimu kwa wachimbaji kufanya kazi katika mazingira salama kwa kutumia vifaa kinga kama kofia ngumu, reflekta, buti, gloves na barakoa (maski). "Ulipuaji wa baruti ni mojawapo ya shughuli...

DKT BITEKO MGENI RASMI NISHATI BONANZA 2025

Image
📌 *Pamoja na kuimarisha afya za Watumishi; Linalenga kuhamasisha ushiriki wa Uchaguzi Mkuu 2025* 📌 *Ni la pili kufanyika tangu kuasisiwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe Dkt Doto Biteko anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Bonanza la Wizara ya Nishati na Taasisi zake litakalofanyika jumamosi Juni 28, 2025 jijini Dodoma. Akizungumzia maandalizi ya Bonanza hilo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Nishati, Bi. Neema Mbuja amesema kuwa, Nishati Bonanza litafanyika kwenye Viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma na kushirikisha taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati na wadau kutoka Wizara nyingine. ‘’ Nipende kuchukua fursa hii kuzikaribisha taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati kushiriki kikamilifu bonanza ambalo linaleta fursa ya kufahamiana na kubadilishana mawazo baada ya muda wa kazi pamoja na kufanya mazoezi ili kujenga afya." Amesema Mbuja Ameongeza kuwa, kwa mwaka huu Nishati ...

NAIBU WAZIRI MKUU DKT. DOTO BITEKO APONGEZWA BUNGENI

Image
  Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko @biteko akifuatilia kwa makini hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhitimisha shughuli za Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 27 June, 2025 Bungeni jijini Dodoma.

TWCC YAWATAKA WAJASIRIAMALI WADOGO WADOGO KUWA NA KAULI NJEMA KWA WATEJA WAO

Image
  Na Madina Mohammed DAR ES SALAAM JAMII HURU  Twcc imeweza kuwapa Mafunzo wajasiriamali mbalimbali na kuwataka pindi wapo Katika biashara zao kuweza kuwazingatia wateja wao hata mteja wanapoulizia biashara kwa kebehi wawe na majibu mazuri ya kuwajibu. Ameyasema hayo Leo Tarehe 27 Juni 2025 Mkurugenzi Mtendaji wa Twcc Dr Mwajuma Hamza Ambapo Leo wametoa wafunzo hayo kwa washiriki wajasiriamali wadogo wadogo ambao wanaenda kushiriki katika maonesho ya 49 ya sabasaba ambayo yanayofanyika Katika viwanja vya sabasaba yanatarajiwa kuanza kesho Tarehe 28 na kutarajia kufanyika Kwa siku 16  Amesema Lengo la maonesho hayo ni kuwa wanapofika Katika maonesho wanatakiwa wabedhi sana Katika kuuza biashara zao Ili kupata mafanikio,"na kusema kuwa siku 16 ni nyingi na wanaporudi mtaani wawe wameshapata wateja wapya,Oda na kupata Fursa mbalimbali. "Kila mwaka huwa tunaandaa Mafunzo haya Kwa makusudi kabisa kuwapa Mafunzo na kuhakikisha wanapata elimu na kujua vitu Gani vinatakiwa upang...

TAMWA YALAANI UDHALILISHAJI WA WANAWAKE WANASIASA MITANDAONI

Image
Na Madina Mohammed DAR ES SALAAM JAMII HURU  Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kimelaani vikali mashambulizi ya kijinsia yanayowakumba wanawake wanasiasa katika mitandao ya kijamii, kikieleza kuwa ni kikwazo kikubwa kwa jitihada za kuendeleza usawa wa kijinsia katika siasa na uongozi. Akizungumza katika Mkutano Mkuu wa mwaka (AGM) wa chama hicho, muasisi wa TAMWA, Halima Sharifu, amesema licha ya mafanikio yaliyopatikana katika nyanja mbalimbali za kijinsia, bado ushiriki mdogo wa wanawake katika siasa ni changamoto kubwa inayoathiri ustawi wa taifa. Sharifu ameongeza kuwa mitandao ya kijamii, licha ya kufungua fursa kwa wanawake kushiriki mijadala ya kisiasa na kujitangaza, imegeuka kuwa jukwaa la mashambulizi ya kisaikolojia na lugha za matusi, dhihaka, na kejeli zenye misingi ya kijinsia. TAMWA imeeleza kusikitishwa na ongezeko la vitendo hivyo vinavyoathiri motisha ya wanawake kushiriki siasa, huku ikisisitiza kuwa jamii inapaswa kushirikiana kuwalinda wanawake dhi...

TANZANIA KUWANIWA VIPENGELE 50 TUZO ZA UTALII DUNIANI 2025

Image
Na Mwandishi Wetu, Dodoma Tanzania imepewa heshima ya kuwa mwenyeji wa hafla ya Tuzo za Utalii Duniani (WTA) kwa Kanda ya Afrika na Bahari ya Hindi mwaka 2025, itakayofanyika Juni 28, 2025 jijini Dar es Salaam na itashiriki kuwania vipengele 50. Akizungumza leo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Dkt. Pindi Chana amesema tukio hilo linaonesha hadhi kubwa ambayo nchi imejipatia kimataifa katika sekta ya utalii. Amesema Tanzania itashiriki katika vipengele 50 vya tuzo hizo, ikiwa ni pamoja na Eneo Bora la Utalii Afrika, Kivutio Bora cha Utalii, Bodi Bora ya Utalii, Hifadhi Bora Afrika, Hoteli Bora kwa Watalii na Kampuni Bora za Safari.  Ameeleza kuwa ushiriki huo ni matokeo ya jitihada za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kupitia filamu ya The Royal Tour na Amazing Tanzania. Amesema zaidi ya washiriki 250 kutoka nchi mbalimbali tayari wamethibitisha kushiriki, wakiwemo viongozi wa sekta ya utalii, wawekezaji, waandishi wa habari wa kimataifa na watoa huduma wa sekta hiyo kutoka Afrika ...

WATUMISHI WA MAGEREZA MANYARA WAPATIWA MAJIKO YA GESI

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  📌Mifumo ya uzalishaji wa bayogesi 126 mbioni kuanza 📌REA, Jeshi la Magereza kununua mashine 61 za mkaa mbadala 📌REA kuwajengea uwezo magereza uendelezaji miradi ya nishati safi 📌Mha. Saidy amewataka magereza kuwa mabalozi wa nishati safi Serikali imewapatia watumishi wa Jeshi la Magereza mitungi ya gesi na majiko ya gesi ya kupikia ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa watumishi na wananchi iliyolenga kufikia malengo yaliyoainishwa kwenye mkakati wa kitaifa wa matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini. Hayo yamebaibishwa leo Juni 26, 2025 na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu wakati wa uzinduzi wa kugawa majiko ya gesi kwa watumishi wa magereza iliyofanyika gereza la Babati mkoani Manyara. Amesema kuwa, katika mkoa wa Manyara tayari Serikali imegawa mitungi ya gesi na majiko ya gesi yapatayo 330 kwa watumishi wa jeshi la magereza na katika gereza la Babati jumla ya majiko ...