Posts

JESHI LA POLISI LATOA TAMKO LA MWENYEKITI WA CCM ALIYEKUTWA AMEKUFA

Image
Kupitia mitandao ya kijamii kunasambazwa picha mjongeo akionekana mtu mmoja mwanaume ambaye anajinasibu kuhusika katika tukio la mauaji ya aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Tawi la Itumbi aitwaye Elia Richard Sambala, miaka 53, mkazi wa Itumbi Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya. Ukweli ni kwamba, Februari 11,2026 saa 7 mchana katika Kijiji cha Itumbi, Elia Richard Sambala, alikutwa shambani kwake akiwa amejeruhiwa kwa kukatwa na kitu chenye makali kichwani na watu wasiojulikana na alifariki dunia muda mfupi baada ya kufikishwa Hospitali ya Wilaya ya Chunya kwa matibabu. Kufuatia tukio hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, kupitia Askari wa kuchunguza matukio ya mauaji, walianza msako mkali na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili kuhusiana na tukio hilo na ufuatiliaji zaidi kwa wengine waliohusika unaendelea. Uchunguzi wa awali umebaini kuwa, chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa masilahi wa eneo la uchimbaji madini ya dhahabu ambapo mmoja wa wanafamilia hao alikodisha kwa wawekezaji raia wa Chin...

JESHI LA POLISI KUENDELEA KUWEKA JITIHADA ZA KUNUNUA MBWA WAPYA WA KISASA WENYE UWEZO WA KUBAINI,KUZUIA NA KUMDHOOFISHA MHALIFU.

Image
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillus Wambura, amesema Jeshi la Polisi litaendelea kuweka jitihada mbalimbali za kununua mbwa wapya wa kisasa na wenye uwezo ili kuboresha muonekano wa mbwa wa Polisi mwenye umbo lenye kumdhoofisha mhalifu. IGP Wambura, ameyasema hayo wakati wa Ufunguzi wa Kikao Kazi cha Wakuu wa Kikosi cha Mbwa na farasi wa Mikoa na Wataalam Waongoza Mbwa na Farasi kikao kilichofanyika jijini Dar es salaam Februari 9,2026 huku akiweka msisitizo kwenye eneo la utoaji wa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa kuwatumia Wanyama kazi katika kudhibiti uhalifu kwenye maeneo yao. Akizungumza na Watendaji hao IGP Wambura, amebainisha kuwa, Kikosi hicho kina umuhimu mkubwa kiusalama kwa kuwa Doria za mipakani na maeneo mengine muhimu hulazimika kutumia mbwa na farasi kwani ni rahisi kupenya kwenye maeneo ambayo gari haliwezi kupita kwa urahisi. Amesema, Jeshi la Polisi lina Mbwa na Farasi wanaofanya kazi katika bandari, viwanja vya ndege na mipakani kwa lengo la kuzuia biashara...

UPENDO NA MAELEWANO VYATAJWA KUWA MSINGI WA AMANI NCHINI

Image
Adam Seleman, Mkazi wa Msongora Jijini Dar Es Salaam amesema tafsiri halisi ya amani ni pamoja na kuelewana na kupendana miongoni mwa Watanzania, akihimiza upendo na maelewano kama msingi wa kudumisha amani na utulivu nchini. Bw. Selemani amebainisha hayo leo Jumamosi Februari 07, 2026 wakati akizungumza na mwandishi wetu wa habari kuhusu umuhimu wa amani kwa ustawi na maendeleo, akisema familia, Jamii na Nchi yoyote inahitaji amani na utulivu ili kuweza kutimiza majukumu na wajibu walionao. "Maana halisi ya amani ni ile hali ya mtu kuwa na uhuru wa kufanya jambo ambalo linaruhusiwa Kikatiba na pia amani tafsiri yake ni upendo, tukipendana ndio amani yenyewe kuanzia ndani ya nyumba. Nawaomba sana tuendelee kushikamana na kudumisha hiki tulichonacho kwani sisi nchi yetu ni kisiwa cha amani." Amesema Bw. Selemani.

AMANI INATUPA UHURU WA KUJIENDELEZA KIUCHUMI- NIACHIENI

Image
Uwepo wa amani katika Taifa kumetajwa kama miongoni mwa rasilimali muhimu zinazohitajika ili kufanikisha malengo na mipango ya mtu mmoja mmoja, Familia, Jamii na Taifa kwa ujumla, Wito ukitolewa kwa Watanzania kuilinda na kudumisha amani. Kauli hiyo imetolewa na Bw. Ramadhan Mohamed Niachieni, Mkazi wa Mtaa wa Mkera, Kata ya Msongora Jijini Dar Es Salaam, akisisitiza kuwa amani ndiyo yenye kuleta maendeleo nchini hivyo kila mmoja anawajibika kuilinda kwa ustawi na maendeleo yetu binafsi. "Amani ina tija sana katika nchi yetu ikiwemo maendeleo ya kila hali kutokana na uhuru wa kufanya shughuli zetu za kiuchumi. Naomba sana tuilinde ili tusiharibikiwe kama wengine na ili tupate fursa ya kuijenga nchi yetu." Amesema Bw. Niachieni. Mwananchi huyo anaungana na maelfu ya wananchi wengine ambao wamekuwa wakisisitiza kuhusu ulinzi wa amani na kuwakataa wote wenye kuhatarisha amani nchini, wakirejea athari za kiuchumi na kijamii zilizojitokeza wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktob...

WITO WATOLEWA, JITIHADA ZA PAMOJA UDHIBITI WA SILAHA HARAMU NCHINI

Image
Kamati ya udhibiti na usimamizi wa silaha imetakiwa kujikita katika utoaji wa elimu kwa jamii kuhusu madhara ya silaha haramu ili kuhakikisha wananchi wanapata uelewa wa kutosha kuhusu matumizi ya silaha haramu. Kauli hiyo imetolewa wakati wa ufungaji wa kikao cha kwanza cha mafunzo cha kamati ya udhibiti na usimamizi wa silaha, kilichofanyika kwa siku tatu Jijini Dar Es Salaam, wajumbe wakikubaliana kuwa ikiwa elimu itatolewa na jamii ikaelewa madhara ya kusambaa kwa silaha haramu, nchi itakuwa salama. Mapema akifunga kikao hicho, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, IGP Camillus Wambura amesema wajumbe wa kamati hiyo ni watu makini na wameonesha kuwa watakuwa msaada mkubwa katika kutekeleza majukumu yao kutokana na kuwa wabobezi katika nyanja tofauti kutoka Serikalini na sekta binafsi. Kwa upande wake Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini na Mrajisi Mkuu wa Silaha DCI Ramadhan Kingai alisema wataendelea kuchukua hatua kali kwa wamiliki wa silaha ambao wamekuwa wakikiuka taratibu z...

POLISI NJOMBE WAKANUSHA TAARIFA ZA ASKARI KUCHOMWA MOTO NA KUPORWA SILAHA

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe katika taarifa yake kwa Vyombo vya habari limekanusha taarifa zilizokuwa zimesambazwa katika Mitandao ya Kijamii nchini zikiambatana na picha mjongeo (Video), zikieleza uwepo wa Askari Polisi wa Mkoa huo aliyechomwa moto na kisha kuporwa silaha Mkoani humo. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Mahamoud Banga, Januari 28, 2026 amesema kuwa katika Mkoa wa Njombe hakuna tukio kama hilo, akionya dhidi ya wanaoandaa na kusambaza taarifa za uongo na upotoshaji. "Jeshi la Polisi linatoa wito kwa baadhi ya wananchi wenye tabia za kuandaa na kusambaza taarifa za uongo na upotoshaji kwa njia mbalimbali kuacha kwani ni kinyume cha sheria za nchi na maadili ya Mtanzania na hakuna faida yoyote kwa wanaofanya hivyo pamoja na familia zao na kwa jamii kwa ujumla." Amesema Kamanda Banga. Polisi pia imesema inaendelea kumfuatilia mtu ama watu waliochukua na kutumia picha mjongeo ya tukio la zamani ambalo a...

MWANACHAMA WA CHADEMA ARUSHA MATATANI KWA KUIBA 'FEDHA ZA LISSU'

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limetangaza kumkamata Bw. Fredrick Mbwambo, Mwanachama wa Chadema na Mkazi wa Arusha kwa tuhuma za wizi wa fedha ambazo alikuwa amezikusanya kutoka kwa wananchi waliokuwa wamechanga kwaajili ya Mwenyekiti wa Chama hicho Bw. Tundu Lissu kupitia Kampeni yao ya "Funga mwaka na Tundu Lissu". Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, SACP Justine Masejo leo Jumatano Januari 28, 2026 Jijini Arusha mbele ya wanahabari, amesema ukamataji wa mtuhumiwa huyo umefanyika baada ya Polisi kupokea malalamiko kutoka kwa Bw. Alute Mughwai, aliyeeleza kubaini wizi wa fedha zilizokuwa zimechangwa. "Ufuatiliaji wa awali umeonesha kuwa ukusanyaji huo wa fedha ulikuwa ukifanywa kupitia namba mbili za simu za makampuni tofauti ya simu na inadaiwa zilihamishwa kwenye namba mbili za simu, moja ikiwa ni ya kampuni ya Tanzania na ya pili ikiwa ni ya kampuni ya simu ya nchi jirani." Amesema Kamanda Masej...

RADA ZA HALI YA HEWA NI MUHIMU KATIKA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA HALI YA HEWA NCHINI.

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) iliandaa warsha ya mafunzo ya Rada za Hali ya Hewa na matumizi ya taarifa zinazotokana na Rada, tarehe 26-27 Januari 2026, Dodoma. Lengo kuu la mafunzo haya ni kuimarisha uwezo wa kitaalamu na kiufundi katika matumizi ya teknolojia Rada, hususan katika uchambuzi, tafsiri na matumizi ya taarifa ili kuboresha utoaji wa utabiri zikiwemo tahadhari za hali mbaya ya hewa kwa wakati na kwa usahihi zaidi.           Mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa warsha hiyo alikuwa ni Mkurugenzi Mkuu wa TMA na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi, Dkt. Ladislaus Chang’a alisema “Kama mnavyofahamu, kwa sasa dunia inashuhudia ongezeko kubwa la matukio ya hali mbaya ya hewa yanayotokana na kuchagizwa na mabadiliko ya hali ya hewa na tabianchi, ikiwemo mvua kubwa, mafuriko, vipindi virefu vya ukame, pamoja na matukio ya vimbunga na upepo mkali. ...

RAIS SAMIA ANAAHIDI NA KUTEKELEZA "NI MFANO SAHIHI KWETU WASICHANA

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametajwa na Wanawake na Mabinti wa Kitanzania kama Kiongozi wa mfano na mwanamke mwenye athari chanya kiasi cha kutoweza kupimika kwa wanawake na mabinti wa Tanzania, Wakimsifu na kumpongeza kwa ujasiri na umahiri wake mkubwa katika kuwaletea maendeleo Watanzania. Kauli hiyo imebainishwa na Bi. Asina Sancho, Kijana na Mjasiriamali wa Kitanzania, akisema Rais Samia amewapa sababu mabinti wengi ya kuamini kuwa wanaweza kufikia malengo yao na kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika kupambania ndoto zao. "Mama Samia ametutia nguvu sisi mabinti kuamini kuwa tunaweza kusimama na kutimiza ndoto zetu, hata katika nyakati za majaribio, Mama Samia ametupa nguvu ya kuamini hakuna linaloshindikana. Katika imani pia Mhe. Rais amesemwa katika namna nyingi mbaya na bado amekuwa na imani na kuwasamehe waliomkosea licha ya wao waliomkosea kutotaka msamaha." Amesema Bi. Sancho...

NISHATI SAFI YA RAFIKI BRIQUETTES IWAFIKIE WATANZANIA WOTE - BALOZI KINGU

Image
*📌Uzalishaji wa Rafiki briquettes uende sambamba na uzalishaji wa majiko banifu* *📌STAMICO waahidi kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa nishati safi nchini* 📍Kisarawe - Pwani Watanzania wametakiwa kuendelea kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutumia nishati safi ya kupikia (mkaa mbadala wa Rafiki briquettes) unaozalishwa na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO).  Rai hiyo imetolewa leo Januari 24, 2026 na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Meja Jenerali Mstaafu Mhe. Balozi Jacob Kingu akiwa ameambatana na Wajumbe wa REB na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) walipotembelea kiwanda cha Nishati safi ya Rafiki Briquettes kinachomilikiwa na STAMICO kilichopo Kisarawe Mkoani Pwani. Balozi Kingu amewataka STAMICO kuongeza kasi ya uzalishaji wa mkaa wa Rafiki briquettes ili watanzani wote nchini waweze kutumia nishati safi ya kupikia na salama.  “Hii ajenda ya matumizi ya nishati safi ambayo kinara wa...

KANISA LA ACK WAIRIMA LASHAMBULIWA KWA MABOMU, GACHAGUA ANUSURIKA

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Makabiliano makubwa yameshuhudiwa katika Kanisa la ACK Wairima, Kaunti ya Nyeri alikokuwa anahudhuria ibada ya leo Jumapili Januari 25, 2026 aliyekuwa Makamu wa Rais wa Kenya Mhe.Rigathi Gachagua Kulingana na mashuhuda wa tukio hilo, Polisi waliokuwa wamefunika nyuso zao wametupa mabomu ya kutoa machozi na kurusha risasi za moto katika kanisa hilo, watu kadhaa wakijeruhiwa huku Gagachua na ujumbe wake wakofanikiwa kutoroka. Hii si mara ya kwanza kwa Naibu huyo wa Rais wa zamani kushambuliwa kanisani ambapo Wiki mbili zilizopita shambulio kama hilo lilitokea nje ya kanisa la Independent Pentecostal Church of Africa (AIPCA) huko Kiamworia, Gatundu Kusini ambapo mafuriko yalitokea baada ya makundi hasimu ya vijana waliokuwa na virungu kuhusika katika vurugu nje ya Kanisa hilo. Kwenye chapisho lake kwenye Mtandao wa X Gagachua amedai kuwa yeye na washirika wake walinaswa ndani ya Kanisa hilo baada ya shambulio hilo kutokana na kile alichokiita Jaribio la m...

𝗠𝗪𝗘𝗡𝗬𝗘𝗞𝗜𝗧𝗜 𝗞𝗔𝗪𝗔𝗜𝗗𝗔: 𝗡𝗜𝗠𝗣𝗢𝗡𝗚𝗘𝗭𝗘 𝗥𝗔𝗜𝗦 𝗗𝗞𝗧. 𝗦𝗔𝗠𝗜𝗔 𝗞𝗨𝗘𝗡𝗗𝗘𝗟𝗘𝗔 𝗞𝗨𝗟𝗘𝗧𝗔 𝗠𝗔𝗘𝗡𝗗𝗘𝗟𝗘𝗢

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Mwenyekiti wa UVCCM na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Mohammed Ali Kawaida amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kuendelea kuleta maendeleo hususani ahadi alizotoa katika kampeni za Uchaguzi Mkuu katika siku 100 za kwanza za uongozi wake. Ndugu Kawaida akizungumza na maelfu ya wanafunzi wa Vyuo vya Kati na Vyuo Vikuu mkoani Dodoma leo tarehe 24 Januari 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete. Ametaja baadhi ya yaliyotekelezwa ikiwemo Bima ya Afya kwa wote na ajira kwa vijana zikiwemo za udaktari.

DKT SAMIA: TANZANIA ITAVUKA NA KUSONGA MBELE

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Waziri Mkuu wa Tanzania, Dkt Mwigulu Nchemba amesema Serikali haitakuwa kikwazo cha kuhakikisha nchi inakuwa moja na inasonga mbele, baada ya kupita katika changamoto. Akizungumza kwa niaba ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, mtendaji mkuu huyo wa Serikali, amesisitiza tayari kuna utashi wa kisiasa wa kujenga umoja nchini na kwamba jukumu hilo amekabidhiwa yeye. Dkt Nchemba ametoa kauli hiyo jijini Arusha leo, Jumamosi Januari 24, 2026 alipotoa salamu za Serikali kwa Rais Dkt Samia, aliyemwakilisha katika maziko ya Gavana wa kwanza wa Tanzania, Edwin Mtei. “Serikali haitakuwa kikwazo cha kuhakikisha kwamba nchi inakuwa moja na tunasonga mbele na mimi niwahakikishie tutavuka na tutasonga mbele na heshima ya Tanzania ya mara zote tutakuwa nayo,” amesema. Amesema Rais Dkt Samia angependa kushiriki maziko hayo, lakini wingi wa majukumu umemfanya amtume yeye kumwakilisha na kwamba yaliyozungumzwa na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini ameyachukua.

MBOWE ATAKA UPINZANI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI, KUJENGA UMOJA WA KITAIFA* ‎

Image
‎Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  ‎Mwenyekiti wa mstaafu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amewataka viongozi wa chama hicho na vyama vingine vya upinzani kushirikiana na Serikali kuleta umoja wa kitaifa. ‎ ‎Katika kulitekeleza hilo, Mbowe amevitaka vyama vya upinzani kuweka utaratibu wa kufanya kazi kwa pamoja ili kuwa katika njia moja ya kuliunganisha Taifa. ‎ ‎Kauli hiyo ya Mbowe inakuja wakati ambao Rais Dkt Samia ameshafanya juhudi mbalimbali zinazolenga kuleta maridhiano ili kujenga mshikamano na umoja wa kitaifa. ‎ ‎Mbowe ametoa kauli hiyo leo, Jumamosi Januari 24, 2026 alipotoa salamu kwa niaba ya familia ya Mzee wakati wa maziko ya Gavana wa kwanza wa Tanzania, Edwin Mtei yanayofanyika mkoani Arusha. ‎ ‎“Tafuteni namna ya kufanya kazi kwa pamoja ili katika utaratibu wa kuliunganisha Taifa, kusiwe na taifa la vipande vipande vya vyama vya siasa,” amesema Mbowe na kuongeza kuwa  ‎ ‎“Tunataka Taifa moja lenye misingi ya maendeleo, lenye upendo, l...

DKT. SAMIA AAGIZA HAYA KUMUENZI MTEI

Image
‎Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  ‎Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameagiza kuharakishwa kwa ujenzi wa barabara ya njia nne ya Tengeru hadi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), kumuenzi Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Edwin Mtei. ‎ ‎Katika hatua hiyo ya kumuenzi Mtei, mkuu huyo wa nchi ameagiza hadi Februari 20, mwaka huu maeneo yote korofi yarekebishwe kuwaondolea wananchi shida na kuleta maendeleo kama alivyotaka marehemu Mtei. ‎ ‎Maelekezo hayo yametolewa na Waziri Mkuu, Dkt Mwigulu Nchemba kwa niaba ya Rais Dkt Samia, jijini Arusha leo, Jumamosi Januari 24, 2026 wakati wa salamu za mwisho kwa Gavana wa kwanza wa Tanzania, Mtei. ‎ ‎Ameitaka Wizara ya Ujenzi na Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), kukamilisha kazi hiyo kwa haraka kama alama kwa Mtei aliyeitumikia nchi kwa uadilifu, heshima na kiu ya maendeleo. ‎ ‎Pia, ameagiza katika Shamba la Mringa Estate ambako mchakato ulielekeza baadhi ya wananchi wanufaike ni muhimu wahusika wote wanaostahili wa...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

WADAU WAJENGEWA UELEWA WA HUDUMA ZA HALI YA HEWA ZINAZOTOLEWA NA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA.

Image
Dodoma Wadau kutoka sekta mbalimbali wamejengewa uelewa wa huduma za hali ya hewa zinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kupitia warsha ya siku mbili iliyofanyika katika Hoteli ya Best Western, Dodoma. Warsha hiyo ilifunguliwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na Makamu Mwenyekiti wa Jopo la Kimataifa la Sayansi ya Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Tabianchi (IPCC), Dkt. Ladislaus Chang’a, tarehe 22 Januari ambapo alisema warsha hiyo inalenga kuimarisha matumizi ya taarifa za hali ya hewa katika sekta zote za kiuchumi na kijamii, na hivyo kuongeza ufanisi na tija katika shughuli hizo. Katika warsha hiyo, wataalamu wa TMA waliwasilisha na kutoa ufafanuzi wa huduma mbalimbali zinazotolewa na TMA, ikiwemo utabiri wa kila siku na tahadhari za matukio ya hali mbaya ya hewa. Wataalamu walianisha pia matakwa ya kisheria kwa WADAU kutumia na kuzingatia taarifa za hali ya hewa katika shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwemo katika sekta ya Ujenzi, usafir...

WATENDAJI WA UCHAGUZI PERAMIHO WATAKIWA KUVISHIRIKISHA VYAMA VYA SIASA

Image
 Na. Mwandishi WETU, Iringa Watendaji wa uchaguzi wametakiwa kuvishirikisha kwa ukaribu vyama vya siasa vyenye usajili kamili katika hatua zote za mchakato wa uchaguzi katika maeneo yao ili kurahisisha utekelezaji wa majukumu. Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele leo tarehe 24 Januari, 2026 mkoani Iringa wakati akifungua mafunzo ya watendaji wa uchaguzi kutoka Halmashauri za Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe. Mafunzo hayo ni sehemu ya maandalizi ya uchaguzi mdogo wa ubunge kwenye Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, mkoani Ruvuma na Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, mkoani Songwe unaotarajiwa kufanyika tarehe 26 Februari, 2026. “Wakati wote wa mchakato wa uchaguzi huu, ni vema mkavishirikisha kwa karibu vyama vyote vya siasa vyenye usajili kamili na wadau wengine wa uchaguzi katika maeneo yenu kuhusu masuala ya kiu...

DK. HOMERA AWEKA MSINGI WA MOTISHA KWA WATUMISHI NAMTUMBO*

Image
- Ataf­siri maono ya Rais Samia kwa vitendo akitoa magodoro 222 - asema motisha ni nguzo ya huduma bora kwa wananchi Na. Mwandishi wetu, NAMTUMBO.  Waziri wa Katiba na Sheria na Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, Dkt. Juma Zuberi Homera, ameendelea kutafsiri kwa vitendo maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ya kuwajengea motisha na mazingira bora ya kazi watumishi wapya, baada ya kukabidhi magodoro 222 kwa watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo, hatua inayolenga kuinua morali na kuongeza ufanisi wa utoaji huduma kwa wananchi. Magodoro hayo yamegawanywa kwa mpangilio mahsusi ambapo 202 kwa watumishi walioajiriwa tayari, 13 kwa watumishi wanaotarajiwa kuajiriwa, na 7 kama akiba.  Makabidhiano yamefanyika tarehe 23 Januari 2026 katika Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Akizungumza mbele ya viongozi wa Serikali na Chama, Dkt. Homera amesema motisha kwa watumishi si hisani bali ni mkakati wa maendeleo, akisisitiza kuwa ajira mpya na usta...

UZINDUZI WA MELI YA MV NEW MWANZA NI UTEKELEZAJI WA MAONO YA RAIS SAMIA- MWIGULU

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Waziri Mkuu wa Tanzania Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba amesema kuzinduliwa kwa Meli mpya ya kisasa ya MV New Mwanza katika Bandari ya Kusini leo Ijumaa Januari 23, 2026 ni dhihirisho la kuendelea kwa utekelezaji wa miradi ya maendeleo kunakofanywa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kama alivyoahidi kwa wananchi. Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu amebainisha hayo muda mfupo baada ya kuzindua meli hiyo, akieleza kuwa kuzinduliwa kwa usafiri huo ni tukio lenye kuonesha pia uwezo wa nchi katika kutekeleza miradi yake ya maendeleo. "Tukio hili tunalolifanya leo la uzinduzi wa meli hii kubwa ni tukio linaloonesha uwezo wetu katika kutekeleza miradi ya maendeleo, linaelezea uwezo wa Kiongozi wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutekeleza maono makubwa yanayoweza kuwaletea Watanzania maendeleo." Amesisitiza Dkt. Mwigulu. Meli hiyo iliyozinduliwa na Waziri Mkuu imejengwa na Mkandarasi kutoka Korea aitwaye Gas Entec Ship-building kwa kushirikiana na TASHICO, ikitengene...