ZOEZI LA KUPIGA KURA LAENDELEA UBUNGO KWA UTULIVU

 






Zoezi la kupiga kura linaendelea kwa utulivu katika kituo cha Buyuni, kilichopo Changanyikeni, Wilaya ya Ubungo, jijini Dar es Salaam, likianza mapema saa 1.00 asubuhi. Wananchi wameendelea kujitokeza kwa utaratibu kutekeleza haki yao ya kikatiba katika mazingira ya amani na usalama.


Maafisa wa tume ya uchaguzi wanaendelea kusimamia mchakato huo kwa weledi, wakitoa huduma kwa wapiga kura kwa namna inayoonesha maandalizi mazuri ya uchaguzi huu.


Wananchi wametakiwa kuendelea kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwa amani, wakizingatia maelekezo yanayotolewa na wasimamizi wa vituo, ili zoezi hilo muhimu kwa demokrasia ya nchi liwe na mafanikio makubwa.





Comments

Popular posts from this blog

IDD AZZAN AJA KIVINGINE TENA JIMBO LA KINONDONI

WANAOSEMEKANA KUWA WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA*

DOLA MILIONI 2 ZA KIMAREKANI Kununufaisha WAKULIMA NCHINI