DK MWINYI MUKINIPA RIDHAA YA KUONGOZA TENA NITAWAWEZESHA MITAJI WAFANYABIASHARA





Mgombea nafasi ya Urais wa Zanzibar kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema endapo akipata ridhaa ya kuiongoza tena Zanzibar kwa kipindi cha miaka mitano atawawezesha mitaji wafanyabiashara.


Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza na wafanyabiashara wa soko la Mwanakwerekwe lilopo wilaya ya Magharibi ‘B’ mkoa wa Mjini Magharibi.


Amesema serikali ya awamu ya nane imetoa sh.bilioni 96 kwa wafanyabiashara mbalimbali ikiwa ni mitaji ya biashara zao.


“Tunatambua kuwa wapo wafanyabiashara waliokuwa bado hawajapata mitaji hiyo lakini kipindi kijacho tunaongeza fungu hilo ili waweze kupata wengi zaidi,” amesema 


Pia, Dk.amesema katika kipindi cha miaka mitano ijayo atajenga masoko mengi Zaidi ikiwemo soko la Kibanda maiti,Kisauni,Fuoni,Kwahaji Tumbo na Mwera ili wafanyabiashara waweze kufanyabiashara na kwamba ataendelea kumaliza changamoto zinazowakabili.










Comments

Popular posts from this blog

IDD AZZAN AJA KIVINGINE TENA JIMBO LA KINONDONI

WANAOSEMEKANA KUWA WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA*

DOLA MILIONI 2 ZA KIMAREKANI Kununufaisha WAKULIMA NCHINI