POLISI YAJIIMARISHA KULINDA RAIA MSIMU HUU WA KRISMASI NA MWAKA MPYA
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, (DCP) David Misime, amesema Jeshi hilo kwa kushirikiana na Vyombo vingine vya ulinzi na usalama vitaendelea kuimarisha ulinzi na usalama wakati na baada ya sikukuu za Krismasi na Mwaka mpya, wito ukitolewa kwa kila mwananchi kutambua na kuheshimu thamani na umuhimu wa amani na usalama kwa kila mmoja. Taarifa iliyotolewa leo Jumatatu Disemba 22, 2025 na Jeshi la polisi imewataka pia wale wote watakaokuwa wakisafiri kutoka eneo moja kwenda jingine kuzingatia sheria za usalama barabarani kama sehemu ya kuepuka ajali za barabarani, wakikumbusha kuhusu kaulimbiu ya wiki ya nenda kwa usalama isemayo "endesha salama, familia inakusubiri." "Maisha yetu na shughuli zetu wakati wa hizi sikukuu yanahitaji mazingira ya amani ili kila mmoha aweze kushiriki kwenye ibada za kumshukuru Mungu, kukaa na familia na marafiki bila ya bugudha yeyote ile hivyo tuilinde amani kwa ushirikiano na kwa nguvu zetu zote." Imesema t...