Posts

TUME YA MADINI YAWAALIKA WADAU KUTUMIA MAABARA YA KISASA

Image
Meneja wa Huduma za Maabara ya Tume ya Madini, Mhandisi Mwarabu Mvunilwa amewaalika wadau wa sekta ya madini nchini kutumia maabara ya kisasa ya Tume kwa huduma za uhakika na viwango vya kimataifa. Akizungumza kupitia mahojiano maalum amesema kuwa maabara hiyo, ipo katika Jengo la TIRDO Complex, Msasani – Dar es Salaam, na imekuwa ikihudumia wachimbaji, wafanyabiashara wa madini, wawekezaji pamoja na taasisi mbalimbali kwa huduma za uchambuzi na ushauri wa kitaalamu. Mhandisi Mvunilwa amesema kuwa maabara hiyo ya serikali imewekewa teknolojia ya kisasa ikiwemo mashine za X-Ray Fluorescence (XRF) na fire assay furnaces zinazotoa matokeo ya haraka, sahihi na yenye gharama nafuu.  “Tunatoa huduma zinazokidhi viwango vya kimataifa vya ISO 17025. Matokeo yetu yanakubalika ndani na nje ya nchi, hivyo kuwa msingi wa uwazi katika biashara ya madini,” amesema. Huduma zinazotolewa na maabara hiyo ni pamoja na uchambuzi wa madini ya metali kwa kutumia XRF, vipimo vya dhahabu na fedha kwa nji...

DKT MWINYI AMEWAHAKIKISHIA WANANCHI WA PEMBA NA UNGUJA KUWA NA UWIANIO SAWA WA MAENDELEO

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU   Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi amewahakikishia wananchi wa Pemba kuwa Serikali itaendelea kuweka uwiano sawa katika miradi ya maendeleo kwa Unguja na Pemba.  Akizungumza leo Septemba, 24 2025 na wafanyabiashara na wajasiriamali wa Soko la Chakechake wa Mkoa wa Kusini Pemba Dk. Mwinyi amesema miradi mbalimbali imekuwa ikitekeleza kwa usawa ikiwemo Sekta za miundombinu, elimu, afya na nyenginezo.  Amesema Serikali itaendelea kulinda na kuimarisha soko la asili la Chakechake ili libakie na uasili wake huku ikipanga kujenga soko jipya la kisasa. "Suala la uwezeshaji wananchi kiuchumi kwa Serikali ijayo itaongeza mara dufu fedha za uwezeshaji ili kuhakikisha kila mjasiriamali anapata mkopo bila kuachwa nyuma," amesema Dk. Mwinyi.  Ameeleza kuwa Serikali itafanyia kazi kwa kina suala la msururu wa kodi na kuweka utaratibu wa kodi nafuu kwa wafanyabiashara.

MBETO:HAMZA HASSAN HANA MPINZANI JIMBO LA SHAURIMOYO

Image
‎Na Madina Mohammed ZANZIBAR  ‎Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar, Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis Mbeto Khamis, leo amezindua rasmi kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika mji wa Zanzibar Magharibi, ndani ya Jimbo la Shaurimoyo, katika harakati za kuimarisha nafasi ya chama hicho katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa hivi karibuni. ‎ ‎Mbeto aliongoza uzinduzi huo akimnadi Mbunge wa sasa wa Shaurimoyo, Hamza Hassan, pamoja na madiwani wa kata zote zilizopo katika jimbo hilo. Akizungumza kwenye hafla hiyo, Mbeto alieleza kwa furaha kwamba Hamza Hassan ameonyesha umahiri mkubwa katika utendaji kazi wake akiwa mbunge, na kwamba amekuwa ni mchapakazi mwenye dhamira ya dhati ya kutumikia wananchi wa Jimbo la Shaurimoyo. ‎ ‎“Hamza Hassan amekuwa akifanya kazi kubwa, si tu kama Mbunge bali pia kama Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Zanzibar. Kazi zake zinajulikana, miradi mingi ya maendeleo imetekelezwa chini ya uongozi wake. Tunajivunia kuwa na kiongozi kama yeye, ...

RC CHALAMILA AKABIDHI MAGARI MAWILI WILAYA YA UBUNGO, KIGAMBONI NA GARI MOJA KWA KIPA WA TAIFA STARS

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Albert Chalamila amekabidhi magari mawili aina ya Land Cruiser Prado yaliyotolewa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kuwawezesha wakuu wa wilaya ya Kigamboni na Ubungo kuwafikia wananchi na kuwahudumia huku pia akikabidhi gari moja aina ya Crown kwa golikipa wa Timu ya Taifa ya Tanzania Yakoub Suleiman kutokana na kazi nzuri aliyofanya kuzuia magoli kwenye mashindano ya CHAN Akizungumza Jijini Dar es salaam wakati wa hafla ya kukabidhi gari hizo hafla ambayo imefanyika katika ofisi za Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Mkuu RC Chalamila amesema magari hayo yametolewa na Rais Dokta Samia ili wakuu wa wilaya waweze kuwafikia wananchi kwa urahisi kuwahudumia na kutatua changamoto za wananchi Aidha Chalamila amemkabidhi Golikipa wa timu ya Taifa ya Tanzania Yakoub Suleiman gari aina ya Crown ikiwa ni ahadi aloyoitoa kwenye mchezo wa robofainali ya mashindano ya CHAN kati ya timu ya Taifa ya Tanzania na Morocco ambapo amesema licha ya kufung...

MAJALIWA KUZINDUA MAONESHO YA TEKNOLOJIA YA MADINI GEITA.

Image
WAZIRI MKUU,Kassim Majaliwa leo Septemba 22, 2025 amefungua maonesho ya nane ya teknolojia ya madini kwa mwaka 2025 ambayo yamefanyika kwenye viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Geita. Maonesho hayo ya Teknolojia ya Madini ambayo yalianzishwa mwaka 2018 yanalenga kuimarisha sekta ya madini nchini na kuhakikisha kuwa rasilimali madini inawanufaisha Watanzania wote.  Maonesho hayo yamekuwa jukwaa mahsusi la Serikali, sekta binafsi, wachimbaji wakubwa na wadogo, taasisi za kifedha, wajasiriamali na wadau mbalimbali wa maendeleo kukutana, kujadili na kubadilishana uzoefu. kaulimbiu ya Maonesho ya Teknolojia ya Madini kwa mwaka huu wa 2025 ni: “Ukuaji wa Sekta ya Madini ni Matokeo ya Matumizi ya Teknolojia Sahihi na Uongozi Bora/Shiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba, 2025.”

DKT. MWINYI AAHIDI MRADI MKUBWA WA MAJI NA KUIMARISHA MIUNDOMBINU KASKAZINI UNGUJA

Image
Mgombea wa Kiti cha Rais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali itajenga mradi mkubwa wa maji ili kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja wanapata maji ya kutosha na ya uhakika. Dkt. Mwinyi alitoa ahadi hiyo leo, tarehe 22 Septemba 2025, alipohutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika Uwanja Shangani, Mkoa wa Kaskazini Unguja. Ameeleza kuwa Serikali imeingia makubaliano na Kampuni ya NEC kutoka Oman kwa ajili ya kufanikisha mradi huo utakaogharimu Dola za Marekani milioni 26, hatua itakayopunguza changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama. Akizungumzia ujenzi wa miundombinu, Dkt. Mwinyi amewahakikishia wananchi kuwa barabara zote kuu na za vijijini zitajengwa kwa kiwango cha lami, ili kuimarisha usafiri na kuongeza fursa za maendeleo vijijini. Aidha, amebainisha kuwa Serikali inaendelea na ujenzi wa Bandari ya Mangapwani ...

SUMVE WAOMBWA KUPIGA KURA NYINGI ZA HESHIMA KWA CCM - DKT. BITEKO

Image
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM, Taifa na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukombe, Ndugu Doto Mashaka Biteko amewahimiza wananchi wa Jimbo la Sumve, wilaya ya Kwimba Mkoani Mwanza kuwapigia kura wagombea wa CCM kwa kuwa Chama hicho kimefanya jitihada kubwa ya kuwaletea maendeleo. Dkt. Biteko amesema hayo Septemba 21, 2025 Mwanza wakati akimnadi mgombea Ubunge wa Jimbo la Sumve kwa tiketi ya CCM, Moses Bujaga ikiwa ni kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu. Amesema Serikali ya CCM imeendelea na jitihada zake za kujenga Kituo cha Reli ya Kisasa ya SGR kwa ajili ya kupokea mizigo itakayosafirishwa kwenda maeneo mbalimbali pamoja na kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa jijini Mwanza ili kufungua uchumi wa mkoa huo kwa ujumla. Aidha, imehakikisha wananchi wa vijiji vyote katika Jimbo hilo wanapata umeme ikiwa ni pamoja na usambazaji umeme katika vitongoji. Dkt. Biteko ameendelea kusema Dkt. Samia Suluhu Hassan ni msikivu na m...