Posts

Showing posts from December, 2025

MARUFUKU KUANDAMANA DISEMBA 09- JESHI LA POLISI

Image
Jeshi la Polisi nchini Tanzania limepiga marufuku maandamano yanayohamasishwa katika mitandao ya kijamii kwa kuyaita maandamano ya amani ya Disemba 09, 2025 kutokana na kutofuata taratibu kulingana na sheria ya Polisi pamoja na kujaa viashiria vingi vya uhalifu na uvunjifu wa sheria na taratibu. Taarifa iliyotolewa leo Ijumaa Disemba 05, 2025 kwa Vyombo vya habari na msemaji wa Jeshi la Polisi David Misime, imesema hatua hiyo imefikiwa pia kutokana na mbinu za kihalifu ambazo zimebainika wakihamasishana kuzitumia kuanzia tarehe 09 Disemba, maandamano hayo yamekosa aifa za kisheria kuyaruhusu kuweza kufanyika. "Mtu yeyote anayepanga kufanya maandamano sheria inamtaka kuwasilisha kwa maandishi notisi kuhusu kufanyika kwa maandamano hayo kwa Afisa Polisi msimamizi wa eneo husika akiainisha sehemu yatakayofanyika maandamano hayo, muda, madhumuni na maelezo mengine kama Waziri atakavyotangaza kwa notisi mara kwa mara kwenye gazeti la serikali." Imesema taarifa ya Polisi. Polisi pi...

DCEA YAPEWA TUZO YA UMAHIRI KATIKA UTAYARISHAJI BORA WA TAARIFA ZA HESABU KWA MWAKA 2024 ‎

Image
‎Na Mwandishi Wetu  ‎ ‎Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekuwa mshindi wa kwanza na kupewa tuzo ya umahiri katika utayarishaji bora wa taarifa za hesabu kwa mwaka 2024 kwa kufuata viwango vya Kimataifa vya Uandaaji wa Hesabu International Public Sectors Accounting Standards (IPSAS) katika kundi la Taasisi za Serikali zinazojitegemea.  ‎ ‎Tuzo hiyo imetolewa tarehe 04/12/2025 na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi (NBAA) katika hafla iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha NBAA APC hotel Bunju jijini Dar es Salaam. ‎ ‎Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya Aretas Lyimo amekipongeza Kitengo cha fedha na uhasibu kwa kufanikisha uandaaji bora wa hesabu uliopelekea kuwa washindi wa tuzo hiyo. ‎ ‎"Niwashukuru watumishi wote wa Mamlaka hasa timu ya fedha na ukaguzi wa ndani kwa kujitoa, kufanya kazi kwa weledi na kuhakikisha kuwa taarifa zetu za fedha zinaandaliwa kwa kiwa...

OFISI YA MSAJILI WA HAZINA YATWAA TUZO YA UANDAAJI BORA WA TAARIFA ZA FEDHA

Image
Na Mwandishi wa OMH Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imeibuka Mshindi wa Pili – tuzo za Uandaaji Bora wa Taarifa za Fedha 2024 (Kundi la Idara za Serikali Zinazojitegemea) kutoka Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA). Tuzo hiyo ilikabidhiwa usiku wa Alhamisi, Desemba 4, 2025, jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Fedha, Laurent Luswetula, ikiwa ni sehemu ya kutambua taasisi zinazozingatia viwango, weledi na uwazi katika uandaaji wa taarifa za fedha za mwaka. Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Mkurugenzi wa Fedha wa Ofisi ya Msajili wa Hazina, Hassan Mohamed, alisema mafanikio hayo yametokana na uandaaji mzuri wa taarifa za kihesabu kwa kufuata miongozo na kanuni.  Aidha, alisema, hilo lisingewezekana bila kujituma kwa watumishi pamoja na uongozi madhubuti wa Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu. Ameeleza kuwa OMH, ikiwemo Kurugenzi ya Fedha na Uhasibu, imeendelea kuimarisha mifumo ya usimamizi, kuongeza ufanisi wa utendaji kazi na kuendelea...

WAZIRI WA NISHATI MHE. NDEJEMBI AZINDUA RASMI MITA JANJA

Image
📌Asema ni mageuzi makubwa ya tekenolojia katika kumuhudumia mteja  📌Aelekeza mita hizo kusambazwa katika maeneo yote yenye uhitaji Waziri wa Nishati Mhe. Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter) yenye lengo la kuboresha na kumrahisishia mteja kufanya manunuzi ya umeme moja kwa moja ikiwa ni mageuzi makubwa ya teknolojia yanayofanywa na TANESCO katika kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma kwa wateja. Waziri wa Nishati amezindua Mita janja hizo Disemba 05, 2025 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, wadau wa sekta ya nishati na watendaji wa TANESCO. Amesema Mita hizo mpya zinamwezesha mteja kupata umeme mara moja baada ya kufanya manunuzi ya token bila kutumia kifaa cha ziada cha kuingiza namba (CIU), hatua inayolenga kupunguza changamoto zilizokuwa zikijitokeza katika mfumo wa zamani. “Leo tunajivunia hatua kubwa ya kihistoria zilifanywa na TANESCO ikiwa ni moja ya kampuni za um...

SERIKALI YASISITIZA KUJENGA MAZINGIRA YAFAAYO KWA WAFANYABIASHARA NA WALAJI KWA KUTUMIA TEKNOLOJIA YA AI-KATAMBI

Image
‎ ‎Na Madina Mohammed  ‎ ‎Serikali imesema kuwa itahakikisha wafanyabiashara wanapata mazingira wezeshi ya biashara, kupata faida, na kuchangia katika ukuaji endelevu wa uchumi wa taifa. ‎ ‎Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mh. Patribas Katambi, alipomuwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara, Mh. Judith Kapinga, katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Ushindani Duniani, yaliyofanyika jijini Dar es Salaam. ‎ ‎Kauli mbiu ya mwaka huu, “Akili Mnemba (AI) katika Kudumisha Ushindani wa Haki na Kulinda Walaji”, inalingana na dhana ya kimataifa ya Artificial Intelligence (AI), Consumers and Competition Policy, ikisisitiza kuwa teknolojia ya AI ni zana muhimu katika kudumisha ushindani wa haki, kulinda maslahi ya walaji, na kuongeza uwazi katika masoko. ‎ ‎“Serikali imejipanga kuwa daraja, si ukuta, kuhakikisha sera zinazolinda walaji na wafanyabiashara zinatekelezwa ipasavyo, hususan katika matumizi ya TEHAMA na AI,” alisema Mh. Katambai, akiweka mkazo katika uwekaj...

MBETO AWATAKA WAAFRIKA WALIOKO NJE KUTUMIA FURSA NA KUWEKEZA TANZANIA

Image
Na Mwandishi wetu,zanzibar Chama Cha Mapinduzi kimewashauri Watanzania wanaoishi Marekani katika Nchi za Falme za Kiarabu na Ulaya kufuata taratibu za kisheria ili kuwekeza miradi ya kiuchumi na Biashara Zanzibar CCM kimeeleza tayari Serikali zake zimeandaa mazingira wezeshi yanayotoa nafasi kwa Watanzania na wageni wenye mitaji ya kuwekeza katika visiwa vya Pemba na Unguja.  Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar, Idara ya Itikadi , Uenezi na Mafunzo ,Khamis Mbeto Khamis ameeleza hayo alipotembelewa na raia toka Canada na Marekani wenye asili ya Afrika.  Mbeto akizungumza na wageni hao ofisini kwake , alitoa wito kwa Watanzania walioko nje na ambao wameshapata uraia wa nchi nyingine,wajitahidi kuwekeza miradi katika Nchi zao za Asili. Alisema kwa Watanzania waliopata uraia wa Mataifa mengine ,wenye mitaji na mipango ya kufanya biashara , wasione woga badala yake ,waje kuja kuwekeza Zanzibar ambako kuna miundombinu ya uhakika.  "Wa...

WATANZANIA WAFURAHISHWA NA META KUZIFUNGIA AKAUNTI ZA MANGE NA MARIA

Image
Wanaharakati Mange Kimambi na Maria Sarungu Tsehai wenye msururu kadhaa wa lawama, malalamiko na kutajwa kuwa sababu ya uvunjifu wa maadili, amani na umoja wa Watanzania wamefungiwa akaunti zao za Meta, kampuni mama ya Teknolojia yenye kumiliki mitandao ya (Instagram, Facebook na WhatsApp). Mange na Maria wanashutumiwa pia kwa kuchochea matukio ya uvunjifu wa amani, mabaya zaidi kuwahi kutokea kwa siku za hivi karibuni nchini Tanzania, Yakifanyika wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali za umma na za binafsi, Wizi, uchomaji moto na vifo vya watu kadhaa kulikotokana na udhibiti wa tukio hilo na umiliki wa silaha kutoka kwa Vituo vya Polisi vilivyovamiwa na Makundi hayo ya kihalifu. Meta imethibitisha taarifa hizo kwa kuandika " Akaunti hizo zimeondolewa kwa kukiuka sera yetu. Haturuhusu watu kuunda akaunti mpya zinazofanana na zile tulizoziondoa awali kwa kukiuka viwango vya juu vya Taasisi ya Meta." Mange na Maria wanatajwa ...

SIMBACHAWENE AWATAKA VIJANA NA WANAHARAKATI KUTAFUTA NJIA SAHIHI YA KUDAI HAKI

Image
  Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene amewataka Vijana na Wanaharakati kutafuta njia sahihi ya kudai haki ikiwemo mazungumzo mezani akiwaasa kuwa vita na vurugu avijawahi kusaidia bali upelekea kupotea kwa amani huku akitolea mfano wa nchi ya Kidemokrasia ya Kongo ambayo takribani ni zaidi ya miaka thelathini wanaitafuta amani ambayo imepotea. Ametoa kauli hiyo wakati wa Mkutano wa Pili unaohusisha Pande Tatu ikiwemo Serikali ya Tanzania, Jamhuri ya Demokrasia ya Congo na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani UNHCR ambapo pia walitumia mkutano huo kusaini nyaraka zinazoelezea Mpango wa Urejeshwaji wa Wakimbizi Elfu Themanini na Sita na Mia Mbili Hamsini na Sita waliopo hapa nchini ambapo pia Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo,Shabani Bihango na Mwakilishi wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani nchini Tanzania,Barbara Dotse waliishukuru Tanzania kwa kuhifadhi wakimbizi hao kwa muda unaozidi miaka thelathini.

TUFUATE TARATIBU ILI KUDUMISHA AMANI YETU- MALECHA

Image
Khalid Malecha, Mkazi wa Kitonga Jijini Dar Es Salaam, ameeleza kuwa maelfu ya wananchi waliathirika moja kwa moja na ghasia na matukio ya uvunjifu wa amani uliojitokeza Oktoba 29, 2025, akihamasisha Jamii kuienzi amani ya Tanzania na kufuata taratibu rasmi za maandamano. Malecha amebainisha hayo leo Alhamisi Disemba 04, 2025 alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, akionesha pia kusikitishwa na waliofanya vurugu hizo kukosa sababu za msingi za kufanya hivyo. "Tuangalie zaidi amani tuliyo nayo katika nchi yetu kwasababu tuna mengi tunayotaka kuyafanya kwente maisha yetu hususani Vijana wenzangu ikiwemo malengo tuliyonayo kwani fursa zipo nyingi ambazo Rais wetu ametuwekea." Amesema Bw. Malecha. Malecha amezungumzia pia matarajio yake katika Wizara mpya ya maendeleo ya Vijana, akisema anaamini kupitia Wizara hiyo Vijana watazifahamu fursa nyingi zaidi za kiuchumi na ajira, suala ambalo litawatoa Vijana katika hatua moja kuelekea nyingine katika ukuaji wa uchumi.

TUTUMIE NJIA YA MAJADILIANO KUONDOA TOFAUTI ZA KIJAMII

Image
Abdulkarim Mohamed, Mkazi wa Dar Es Salaam amesema kufanya vurugu kama sehemu ya kushinikiza serikali kutoa haki ama huduma fulani kwa jamii hakuna faida yoyote na badala yake vurugu zimekuwa sababu ya anguko la kiuchumi na kukwama kwa shughuli za kijamii na kiuchumi. Mohamed amebainisha hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelezea uzoefu na athari ya kiuchumi na kijamii aliyoipata wakati wa vurugu na matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, akilaani wale wote walioratibu na kushiriki katika matukio hayo ya uvunjifu wa amani. "Kwa mimi binafsi siliungi Mkono, sisi Tanzania tumezoea kuwa ni nchi ya amani na hao waliopanga jambo hili mapema kulingana na kauli zao hatukuamini kama jambo lile lingetokea na bado mpaka sasa tuna mashaka ikiwa kweli walikuwa ni Watanzania waliofanya matukio haya." Amesema Bw. Mohamed. Kadhalika Bw. Mohamed amehimiza pia kufuatwa kwa taratibu rasmi zinazokubalika kisheria na kijamii ikiwa baadhi ya ...

ELIMU YA MBOLEA YAONGEZA TIJA KILIMO CHA PAMBA SIMIYU*

Image
Afisa Udhibiti Ubora Mwandamizi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Godwin Vedastus akitoa elimu ya mbolea kwa wakulima wa kijijichi Bukangilija kilichopo Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu leo tarehe 3 Desemba,2025. Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anamringi Macha akiwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Wizara ya Kilimo, Idara ya Maendeleo ya Mazao Samson Poneja walipotembelea ofisini kwake kueleza uwepo wao mkoani humo kutekeleza kampeni ya Mali Shambani tarehe 3 Desemba, 2025 Wakulima wa kijiji cha Hinduki kilichopo Halmshauri ya Wilaya ya Maswa Mkoani wa Simiyu wakifuatilia mafunzo ya matumizi sahihi ya mbolea tarehe 3 Desemba, 2025 ikiwa ni utekelezaji wa kampeni ya Mali Shambani yenye lengo la kutoa elimu ya matumizi sahihi ya pembejeo za kilimo, kuhamasisha wakulima kupima afya ya udongo na kujisajili kwenye mfumo wa pembejeo za kilimo ili kunufaika na ruzuku ya mbolea na mbegu inayotolewa na Serikali. Diwani wa Kata ya Sukuma Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu, Mary Sagana Misangu...

TWIGA STARS YAKABIDHIWA TSH MILIONI 50

Image
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa, amekabidhi Shilingi Milioni 50 kwa timu ya Taifa ya Wanawake (Twiga Stars) kama pongezi kutoka kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufuzu mara mbili mfululizo Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON) 2026. Makabidhiano hayo yamefanyika leo Desemba 3, 2025 jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya Serikali kutambua juhudi na nidhamu ya wachezaji pamoja na benchi la ufundi katika safari yao ya kufuzu michuano hiyo mikubwa barani Afrika, inayotarajiwa kufanyika Morocco mwaka 2026.

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

KINACHOHAMASISHWA DISEMBA 09 SI MAANDAMANO YA AMANI- POLISI

Image
Jeshi la Polisi nchini Tanzania kwa kushirikiana na Vyombo vingine vya Ulinzi na usalama limesema linaendelea kufuatilia kwa karibu yanayoendelea kwenye Mitandao ya Kijamii na kwenye makundi sogozi wakihamasisha wanayoyaita maandamano ya amani yasiyo na kikomo ya Disemba 09, 2025. Polisi pia imeeleza katika taarifa yake kwa Vyombo vya habari leo Jumatano Disemba 03, 2025 kuwa linaendelea kuzuia uhalifu sambamba na kuwakamata wale wanaofanya makosa mbalimbali ikiwemo ya Kimtandao kwa wale wanaoendesha makundi mbalimbali katika Mitandao ya kijamii ya kuhamasisha uhalifu na kuwachukulia hatua kulingana na sheria za nchi. Msemaji wa Jeshi la Polisi David Misime katika taarifa hiyo amelaani pia kile kinachoelezwa katika makundi hayo ya mitandao ya Kijamii ikiwemo wito wa kutoshika silaha katika maandamano hayo ikiwa mwandamanaji hakupitia mafunzo na badala yake waaachie silaha wenye mafunzo. "Kupitia Mitandao na Klabu mbalimbali za Mtandaoni wanahamasishana pia kusiwe na shughuli nying...

WABEBA ZEGE WAYAKATAA MAANDAMANO YA DISEMBA 09, "TUMECHOKA"

Image
WAKATI joto la maandamano ya Disemba 09 likizidi kupanda, mjadala wa kuyapinga na kuyakataa maandamano hayo umeendelea Kila Kona, huku vijana, wazee na wanawake wakieleza kuwa wasingependa kilichotokea Oktoba 29 kijirudie tena. Hawa hapa ni Vijana waliokuwa katika Shughuli zao za Kujitafutia mkate wa kila siku kama ambavyo inaonekana kwenye Video hii maongezi yao yaliyonaswa hapa ni kuhusu kupinga vikali kujihusisha na masuala ya maandamano huku wakilinganisha athari ambazo wamezipata Oktoba 29. "Tumechoka na maandamano tumekaa ndani siku tatu tunachokula chamaana hakuna hiyo Tarehe 09 hatuyawezi tumechoka maandamano " Mwananchi wa Dar es Salaam.

Bara la Afrika: Tunahitaji wanahabari mahiri kukuza sayansi, teknolojia na ubunifu

Image
Na Veronica Mrema - Pretoria  Uandishi wa habari za sayansi kwa umakini na umahiri ni nyenzo muhimu ili kufikisha ujumbe sahihi kwa jamii, kusaidia kukuza maendeleo ya tafiti na vumbuzi mbalimbali. Bara la Afrika bado lina uhitaji mkubwa wa waandishi wa habari ambao wamejikita na wapo na umahiri katika kuwasilisha masuala ya sayansi kwa lugha rahisi zinazoeleweka kwa jamii. “Kazi yoyote ile tunayoifanya [katika] sayansi ina maana tu pale inapofahamika vizuri kwa watu na jamii nzima,”. Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu wa Afrika Kusini Profesa Blade Nzimande amesema hayo alipokuwa akifungua rasmi Mkutano wa 13 wa Waandishi wa Habari za Sayansi Duniani. Mkutano huo WCSJ2025 unafanyika Pretoria Afrika Kusini kuanzia Disemba 1-5, 2025 ukiwa na kauli mbiu isemayo 'Uandishi wa sayansi, unaojenga uelewa na uthabiti wa sayansi na haki za kijamii'. “Nilipoombwa kuja kufungua mkutano huu nilikubali mara moja kwa sababu ya umuhimu wa nafasi ya waandishi wa habari za sayansi katika ...

BEI ZA MAFUTA DESEMBA 2025: PETROL I YAENDELEA KUSHUKA

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  DODOMA: Mamlaka ya Ushibiti wa Huduma za Nishati na Maji ( EWURA) imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta aina ya petroli zitakazotumika hapa nchini kwa mwezi Desemba 2025, zikionesha kuendelea kushuka kwa bei ya petroli.  Ahueni hiyo inatokana na kupungua kwa gharama za kuagiza mafuta katika bandari ya Dar es Salaam kwa wastani wa 2.4% kwa petroli, na 3.6% kwa mafuta ya taa.  Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Mwainyekule, leo 3 Desemba 2025, imebainisha kuwa, bei ya rejareja ya petroli imepungua kwa shilingi 2.38 (Dar es Salaam), 2.26 (Tanga) na shilingi 2.45 kwa Mtwara. Aidha, bei ya mafuta ya taa kwa Dar es Salaam imepungua kwa shilingi 120.48 ikilinganishwa na bei za mwezi Novemba 2025.  Hivyo basi, bei za reja reja za petroli kwa mwezi huu, zitakuwa shilingi 2610.10, 2616.13 na 2616.24 kwa Dar es Salaam, Tanga na Mtwara mtawalia. Kwa upande wa dizeli, Dar es Salaam ni shilingi 2639.54, Tanga 2648.86 na ...

KARNE YA AI: 'SADC BADO KUNA PENGO LA MAWASILIANO YA SAYANSI'

Image
Na Veronica Mrema - Pretoria  Ulimwengu wa sayansi na teknolojia unasonga kwa kasi ya ajabu. Mataifa makubwa duniani yanawekeza kwenye ubunifu, utafiti wa kisayansi, na teknolojia za kisasa. Teknolojia kama akili unde, kilimo cha kisasa na tiba za kibunifu zaidi zinabadilisha maisha katika mataifa makubwa duniani. Karne ya akili unde [AI], roketi zinavuka anga, kuna uvumbuzi na gunduzi nyingi katika teknolojia mpya kwa kasi ambayo dunia haijawahi kushuhudia. Mataifa makubwa yanawekeza, yanashirikiana, na yanapasha habari za sayansi kwa umma wao kwa kasi. Lakini upande mwingine wa dunia, ndani ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika [SADC], bado kuna pengo kubwa katika mawasiliano ya sayansi.  Watafiti wanagundua, Serikali zinafanya miradi, taasisi zinavumbua, lakini taarifa 'hazitembei' kwa kasi inayohitajika. Bado haziwafikii vema wananchi wake, hazijengi uelewa na hazifanyi sayansi kuwa sehemu ya maisha ya kila siku. Ndani ya SADC, bado kuna pengo kubwa kati ya maendeleo y...

MBETO: RAIS SAMIA AMETHIBITISHA UZALENDO NA UUNGWANA ALIONA.

Image
 Na Mwandishi Wetu, Zanzibar  Chama Cha Mapinduzi kimesema hotuba iliotolewa na Rais Dk Samia Suluhu Hassan alipozungumza na Wazee wa Mkoa wa Dar Es Salaam ,ameonyesha kina cha uelewa alionao, ukomavu na uungwana wake kisiasa . Pia CCM kimeitaja hotuba hiyo imeshiba uzalendo, historia na yenye kuhimiza haja na nia ya kuendeleza dhima ya Umoja wa Kitaifa . Hayo yameelezwa na Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar , Idara ya Itikadi , Uenezi na Mafunzo, Khamisi Mbeto Khamis aliyeitaja hotuba hiyo kuwa imeweka msimamo thabit wa kulinda uhuru , Amani na utulivu. Mbeto alisema matamshi ya Rais Dk Samia yamewataka viongozi wa madhehebu za Dini kuacha kuingilia medani za Siasa na kuipangia hatma Serikali na kusisitiza kuwa Tanzania haina Dini bali wananachi wake ndio wenye imani za Dini.  Alisema hotuba hiyo ya Rais licha ya kuwa ni ya kizalendo ,imetoboa ukweli unaowataka Watanzania wote kujiona wako sawa mbele ya katiba na kuwatak...

RAIS SAMIA AYASHUKIA MATAIFA YANAYOIPANGIA TANZANIA LA KUFANYA " WHO ARE YOU?

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa Tanzania ni huru na haitoingiliwa na serikali ama chombo kingine chochote kutoka nje ya Tanzania, akisema fedha chache wanazozitoa kwa Tanzania si kigezo cha kuingilia mambo ya Tanzania. Dkt. Samia ameyasema hayo leo Jumanne Disemba 02, 2025 Jijini Dar Es Salaam alipozungumza na wazee wa Mkoa wa Dar Es Salaam, akisisitiza kuwa Tanzania imeumbwa vizuri na kuwekwa pazuri katika soko na siasa za dunia na ndilo tatizo linalosababisha kupigwa vita. "Nje huko wanakaa kuwa Tanzania ifanye hili na hili halafu ndiyo itakuwa hivi, who are you? Niwaulize ndugu zangu, kwao hayatokei? Tumenyanyua sauti sisi kusema ya kwao? Wanadhania kuwa bado wao ni master wetu, ni wakoloni kwetu? Kitu gani? Ni fedha chache wanayotugaia? Na fedha yenyewe sasa hivi haipo, tunafanya biashara wao wapate na sisi tupate." Amekaririwa Rais Samia. Rais Samia amesema Tanzania kutofungamana na upande wo...

KAMA HUMPENDI SAMIA KUTOKANA NA DINI YAKE, SUBIRI AMALIZE MUDA WAKE- RAIS SAMIA

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  "Mimi toka nimeingia madarakani matamko nane yametolewa na Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), lakini ukienda chini huko wenyewe wanapingana kwamba matamko yale hayafanyi vizuri kwasababu waliosimama kwenye mstari wa haki wanaona ile ni batili inayofanyika. Kwahiyo niseme kwamba Tanzania yetu ni nchi ya umoja, mshikamano, amani na utulivu na ndio ngao zetu, tusivurugwe ndugu zangu kupitia mirengo ya dini, siasa ama mirengo mingine yoyote ile hata kama aliyepo juu serikalini humtaki. "Kuna muda, hii ni nchi ya demokrasia, huyo mtu ataongoza mpaka wakati huu, kafanya makosa semeni makosa yake. Kosa la serikali ya awamu ya sita ni kueneza huduma bora za afya kwa Watanzania? Kosa letu kueneza huduma bora za elimu mpaka kule Vijijini? Kosa letu kukuza uchumi wa Tanzania ukakua mpaka kusifiwa duniani?, Kosa letu ni kuifanya Tanzania kuwa salama na ikalike? Kosa letu ni nini? Kama mtu hampendi anayeongoza tustahimili tu, mioyo yetu ime...

RAIS SAMIA HAJAPUUZA MANENO, USHAURI NA HISIA ZA WANANCHI- CHALAMILA

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mhe. Albert John Chalamila amempongeza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwa imara katika kuunda serikali, bila kupuuza maneno, ushauri na hisia za Watanzania. Chalamila amebainisha hayo leo Jumanne Disemba 02, 2025 wakati Rais Samia Suluhu Hassan akikutana na Wazee wa Mkoa wa Dar Es Salaam, katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere, akimpongeza pia kwa kuunda Wizara mpya ya maendeleo ya Vijana kwa kutambua kuwa Vijana ndiyo nguvu kazi ya Taifa la Tanzania. "Mhe. Rais sisi wana Dar Es Salaam tumekusikiliza siku ukiapishwa, tumesikiliza hotuba yako ya kwanza Bungeni, maelekezo yako yote tumeyatekeleza na tunaendelea kuyatekeleza kwa kuhakikisha tunafanyia kazi kwa kusikiliza makundi yote ya msingi, hisia zao, kwa kusikiliza matatizo yao ili tuyafanyie kazi na kuunda taifa lenye umoja." Amesema Chalamila. Katika hatua nyingine, Mhe. Chalamila ameeleza kuwa Rais Samia kukutana na Wazee wa Dar E...

‎MAADHIMISHO YA WIKI YA USHINDANI: TEKNOLOJIA YA AKILI MNEMBA (AI) NA ATHARI ZAKE KATIKA USHINDANI WA MASOKO ‎

Image
Na Madina Mohammed DAR ES SALAAM JAMII HURU  ‎Tume ya Ushindani ya Tanzania (FCC) imeanza maadhimisho ya Wiki ya Ushindani ikiwa na lengo la kuongeza uelewa wa umma kuhusu athari za teknolojia ya Akili Mnemba (AI) katika ushindani wa masoko. Maadhimisho haya yanaendelea kuzingatia Siku ya Ushindani Duniani, ambayo kilele chake kitatimia Desemba 5, 2025. ‎ ‎Akizungumza jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, alisema kuwa maadhimisho haya ni sehemu ya utekelezaji wa uamuzi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa la mwaka 1980, ambalo liliamua kuanzisha maadhimisho ya kimataifa yanayolenga kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa ushindani katika masoko duniani. Uamuzi huu ulileta kanuni za kudhibiti vitendo vinavyokandamiza ushindani, maarufu kama The UN Set, ambazo sasa ni msingi wa sera na mifumo ya ushindani duniani kote. ‎ ‎Uchumi wa Kidigitali na Changamoto za AI ‎Bi. Ngasongwa alisema kuwa FCC inajitahidi kuhakikisha kuwa masoko ya Tanzania yanabaki huru,...

TUTAPONYA WAATHIRIKA WA MATUKIO YA OKTOBA 29, 2025

Image
Jaji Mkuu mstaafu na Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 Mohammed Chande Othman amesema katika kutekeleza wajibu wa Tume hiyo, wanatarajia kuponya waathirika wa vurugu hizo pamoja na watuhumiwa wa matukio hayo ya Oktoba 29. Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Disemba Mosi, 2025, Jaji Chande amesema watawatafuta walioshiriki, Vyama vya siasa, asasi za kiraia, wasimamizi wa uchaguzi na Tume huru ya Taifa ya uchaguzi, Viongozi wa dini na Watu wengine ili kuzungumza nao kuhusu matukio hayo. Aidha pia ameeleza kuwa watazungumza pia na wajasiriamali, wafanyabiashara, watu mashuhuri, mamlaka za serikali za mitaa katika maeneo yaliyoathirika, Vyombo vya ulinzi na usalama, wanahabari na sekta binafsi pamoja na washirika mbalimbali wa maendeleo.

WATANZANIA WANATAKA UWAZI NA UCHUNGUZI KAMILI- JAJI OTHMAN CHANDE

Image
Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 Jaji Mkuu mstaafu Mohammed Chande Othman amesema Watanzania wanataka uchunguzi kamilifu wa Matukio ya Oktoba 29 pamoja na kutaka uwazi kwenye kutekeleza wajibu wao. Jaji mstaafu Othman amebainisha hayo leo Jumatatu Disemba Mosi, 2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari, akisisitiza kuwa baadhi ya Mikutano yao wataifanya hadharani na mingine faragha ili kulinda haki za watu wengine. "Mikutano yetu mingine itafanyika kwenye hadhara na mingine itabidi tuende kwenye faragha kwenye mazingira maalumu ili kulinda haki za mtu na Tanzania sasahivi tuna sheria ya kulinda faragha za watu." Amesema Jaji Othman. Mwenyekiti huyo wa tume ameeleza kuwa matakwa hayo ya watanzania wameyapokea na ndiyo watakayoyatumia katika kujibu hadidu za rejea katika utekelezaji wa majukumu yao ya uchunguzi wa matukio hayo ya Oktoba 29, 2025.