Posts

Showing posts from December, 2025

TUSHEHEREKEE MWAKA MPYA PASIPO KULETA TAHARUKI YOYOTE:RC CHALAMILA ‎

Image
‎Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  ‎Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert John Chalamila, amewasihi wananchi pindi wanaposheherekea sikukuu za mwaka mpya pasipo kuleta taharuki yoyote na pia ametoa wito kwa wakazi wa mkoa huo kusherehekea Mwaka Mpya kwa njia zisizozua taharuki kwa wengine. ‎ ‎Akizungumza na waandishi wa habari Leo 31,2025 Mkuu wa mkoa Albert Chalamila amesema kuwa tabia ya kupiga fataki kiholela na kuchoma matairi wakati wa shamrashamra za Mwaka Mpya inaweza kuleta usumbufu, hofu na hata kuathiri usalama wa wananchi, hasa ikizingatiwa hali ya kiusalama ambayo jiji hilo limepitia miaka ya nyuma. ‎ ‎Amesisitiza kuwa kwa yeyote anayehitaji kulipua fataki ni lazima kupata kibali maalumu kutoka kwa Jeshi la Polisi, huku akibainisha kuwa maofisa wa usalama watakuwepo eneo la tukio kuongoza utaratibu na kuhakikisha kunafuatwa sheria na taratibu. ‎ ‎“Ni muhimu kuwaheshimu majirani na kuwapasha taarifa mapema endapo utalipua fataki ili kuepusha hofu au taharuki isiyo ya la...

RC CHALAMILA:SHULE ZIPO TAYARI KUPOKEA WANAFUNZI 2026 ‎

Image
‎Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  ‎MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amewataka wanafunzi wote waliopangiwa kuanza kidato cha kwanza kuwa tayari kuanza masomo ifikapo Januari mosi, 2026. ‎ ‎Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa, Chalamila amesema maandalizi ya ufunguzi wa shule yamekamilika kwa asilimia kubwa, huku akisisitiza kuwa changamoto za miundombinu zilizokuwa zikijitokeza miaka ya nyuma zimeshapatiwa ufumbuzi. ‎ ‎Amesema mkoa unatarajia kupokea jumla ya wanafunzi 95,323 watakaoanza masomo ya sekondari, huku Serikali ikihakikisha kuwa miundombinu ya madarasa na samani (madawati) inakidhi idadi hiyo bila kuwepo kwa vikwazo. ‎ ‎"Dar es Salaam tuko tayari. Maandalizi yote yamekamilika na hakuna mwanafunzi atakayekosa nafasi au kusoma katika mazingira magumu. Tunatarajia kupokea wanafunzi zaidi ya 95,000 na kila mmoja atapata haki yake ya elimu kama ilivyopangwa," alisema Chalamila. ‎

RC CHALAMILA:MIILI KUANZA KUTOLEWA BILA MALIPO

Image
  Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  SERIKALI imesisitiza kuwa miili ya wagonjwa wanaofariki dunia wakiwa wanapatiwa matibabu hospitalini, itatolewa bila malipo na kwa haraka ili kuwawezesha ndugu na jamaa kufanya taratibu za mazishi bila usumbufu. ‎ ‎Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ametoa agizo hilo leo jijini hapa alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu maboresho ya huduma za jamii na usimamizi wa utu wa binadamu. ‎ ‎Chalamila amesema hatua hiyo inalenga kupunguza changamoto zinazowakumba wananchi katika kipindi cha majonzi, hususan wale wanaokosa uwezo wa kugharamia huduma mbalimbali baada ya kufiwa na wapendwa wao. ‎ ‎"Lengo ni kuhakikisha wananchi hawapati usumbufu wa ziada wanapokuwa katika kipindi kigumu cha kuondokewa na ndugu zao. Mwili unapaswa kutolewa mara moja ili taratibu za mazishi ziendelee," amesema  Chalamila

POLISI YASISITIZA KUSHEREHEKEA MWAKA MPYA KWA KUZINGATIA USALAMA NA AMANI

Image
 *_Yapiga Marufuku uchomaji wa matairi na upigaji fatati usiokuwa na vibali_* Jeshi la Polisi nchini Tanzania limetoa wito kwa wananchi kusherehekea sikukuu ya mwisho wa mwaka na kuukaribisha mwaka mpya kwa kuzingatia sheria na kuzingatia kanuni za kiusalama, likisisitiza kuwa imara katika kuimarisha usalama kwa misingi ya sheria. Aidha Polisi imetoa rai kwa kila mzazi kuzingatia ulinzi kwa watoto kama sheria, kanuni na taratibu zinavyoelekeza ili kuwaepusha na madhara mbalimbali ikiwemo kupotea kama ilivyoshuhudiwa katika sikukuu nyingine zilizopita. Taarifa ya Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania David Misime kwa Vyombo vya habari imesisitiza pia kwa watumiaji wa Vyombo vya moto na watumiaji wa barabara kuzingatia na kutii sheria za usalama barabarani na kuongozwa na kaulimbiu ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani isemayo "Familia yako inakusubiri zingatia usalama." "Kulingana na desturi zetu kama Watanzania huwa tunakuwa na shughuli mbalimbali katika kuhitim...

MALISA AMETHIBITISHA WANAOHAMASISHA VURUGU SIO WATANZANIA - MCHANGE

Image
 ‎ Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Suala la Thadei Kweka lafichua hatari ya watu walioukana uraia kuingilia masuala ya ndani ya Taifa ‎ ‎Taarifa iliyotolewa na Malisa Godlisten akidhani analichafua jeshi la polisi kumkata Mtanzania aliyeukana utanzania na kuwa mmarekani Thadei Kweka imeweka wazi ukweli mzito unaopaswa kuangaliwa kwa jicho la Taifa kuwa watu wanaohamasisha vurugu,uchochezi na uvunjifu wa amani si Watanzania, na hata watanzania wachache hawaishi Tanzania kama inavyozidi kubainika  ‎ ‎Kwa mujibu wa taarifa ya Malisa , Thadei Kweka anayetajwa katika sakata hilo sio raia wa Tanzania, bali ni raia wa Marekani aliyeukana uraia wa Tanzania, na aliingia nchini kwa Tourist Visa ya muda wa siku 90.  ‎ ‎Huu ni uthibitisho wa wazi kwamba mhusika hakuwa nchini kama Mtanzania, bali kama mgeni ambaye kipindi akiwa marekani alikuwa anatukana serikali, anashawishi vurugu na uchochezi huku watanzania hasa vijana wakijua ni mwenzao . ‎ ‎Ifahamike kuwa Uraia wa nchi si hat...

KUELEKEA MWAKA MPYA 2026,REA YAWASHIKA MKONO WAHITAJI

Image
 * 📍Hombolo - Dodoma Kuelekea Mwaka Mpya 2026, Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imewagusa Watanzania wenye mahitaji mbalimbali kwa kutoa mkono wa faraja na kuwatakia heri ya mwaka Mpya ujao. Zoezi la kuwapatia mahitaji walemavu limeongozwa na Bi. Judith Abdalah kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa REA mha. Hassan Saidy ambapo REA imetoa mahitaji mbalimbali kwa Kikundi cha Walemavu wa Ukoma waliopo Kata ya Hombolo jijini Dodoma.  Akiwasilisha salamu za REA, Bi. Abdalah amewataka walemavu wa Ukoma kuishi kwa upendo na amani na kusisitiza kuwa, REA itaendelea kuwashika mkono kwa kuwapatia mahitaji mbalimbali ili wakue kiuchumi na kijamii.  Halikadhalika, Swalehe Kibwana Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi Tawi la REA (TUGHE), amesema zoezi hilo la kuwafikia na kuwasaidia wahitaji mbalimbali ni endelevu na REA itaendelea kutoa mahitaji kwao hususan kwa walemavu wa ukoma waliopo Hombolo.  Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kikundi cha Wanawake na Samia mkoa wa Dodoma Bi. Fatuma ...

WAUMINI KATOLIKI WAZIDI KUWAPINGA KITIMA, RUWAICHI

Image
Dar es Salaam. Upinzani wa waumini wa Kanisa Katoliki dhidi ya mwenendo wa baadhi ya viongozi wa juu wa kanisa, akiwemo Padri Dkt. Charles Kitima na Askofu Mkuu Ruwa’ichi, unaendelea kushika kasi, huku hoja za kimaadili, kisheria na kiteolojia zikiwekwa wazi hadharani. Kupitia tafakuri nzito ya dhamiri iliyotolewa na Mwalimu Ludovick Joseph, muumini wa Kanisa Katoliki nchini Tanzania, waumini wameanza kujenga hoja ya pamoja kwamba Kanisa si mtu mmoja, si padri wala askofu, bali ni jumuiya ya waumini, na kwamba viongozi wa kanisa hawako juu ya Injili wala juu ya waumini. Katika tafakuri hiyo, waumini wanasema wazi kuwa kuhoji, kukosoa na kuomba uchunguzi dhidi ya kiongozi wa kanisa si uasi, si dhambi wala si chuki, bali ni haki ya kisheria inayotambuliwa ndani ya mfumo wa Kanisa Katoliki lenyewe. “Kanisa ni takatifu kwa sababu ya Kristo, lakini viongozi wake ni wanadamu wenye mipaka na wanaweza kukosea,” inaeleza tafakuri hiyo, ikisisitiza kuwa hakuna kiongozi aliye juu ya Injili. MATUS...

DKT MWIGULU NCHEMBA AUNGA MKONO UJENZI WA KITUO CHA DALADALA BUNJU B

Image
  Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mwigulu Nchemba ameridhia ujenzi wa Kituo cha Daladala Bunju B, Kata ya Mabwepande Wilaya ya Kinondoni Mkoa wa Dar es Salaam ambapo ujenzi huo utagharimu kiasi cha shilingi Bilioni 2.3. Akiongea wakati wa ziara aliyoifanya leo Disemba 29, 2025 wakati akitembelea Soko la Bunju B pamoja na kusikiliza kero mbalimbali za Wananchi, waziri Mkuu amesema kuwa amepokea wazo la uhitaji wa ujenzi wa Kituo cha daladala na ameahidi kuwa hitaji la fedha kiasi cha shilingi Bilioni 2.3 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa stendi hiyo haraka itapatikana. "Nakubaliana nanyi na naunga mkono ujenzi wa Stendi hii kwani itakwenda kuongeza kasi na mzunguko wa Biashara katika eneo hili la Bunju B" Alisema Dkt Mwigulu. Sanjari na hilo amesisitiza kuwa kituo hicho cha daladala ujenzi wake utakwenda sambamba na miundombinu ya Barabara, Soko na Maduka ili kuwa na mzingira rafiki ya Kibiashara ambayo yatapelekea kuinua kipat...

SERIKALI YAIPELEKA NIDA KIDIGITALI,LENGO KURAHISISHA UTOLEWA WA VITAMBULISHO

Image
Na Mwandishi Wetu, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, amezindua namba maalumu, itakayotumiwa na wananchi kufuatilia kitambulisho cha taifa baada ya kuwasilisha maombi ya kitambulisho hicho, hali itakayopelekea wananchi kupata na kujua taarifa za maombi ya kitambulisho kwa kutumia namba maalumu hiyo. Amezindua namba hiyo maalumu, leo jijini Dar es Salaam, ambapo amesema vitambulisho vingi vimezalishwa na tayari vimepelekwa sehemu husika, ikiwemo wilayani ambapo muombaji wa kitambulisho alijiandikishia na bado wahusika awajafuata kadi zao hali inayopelekea baadhi ya wananchi kukosa huduma mbalimbali huku akizitaja huduma za afya, mafao ya ustawi, usajili wa wanafunzi katika vyuo mbalimbali samabamba na maombi ya mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu(HESLB). “Hivi leo tunavyozungumza katika wilaya zetu zote nchini, viko vitambulisho vingi sana ambavyo havijachukuliwa na sababu kubwa inakua kwamba muombaji hajui kitambulisho chake kipo katika hatua gani, kup...

DKT. MWIGULU AKAGUA HALI YA UZALISHAJI NA USAMBAZAJI WA MAJI RUVU CHINI

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 29, 2025 amekagua hali za uzalishaji na usambazaji wa maji eneo la Ruvu Chini, mkoani Pwani. Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa maji unaotokana na mabadiliko ya tabia ya nchi, Serikali ilianza utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita. “Mipango hii ya ujenzi wa miradi inayolenga kukabiliana na changamoto ya upungufu wa maji ilianza muda mrefu, Serikali iliona na ilianza kutafuta majawabu ya hali hii miaka mitatu iliyopita kwa kujenga miradi mikubwa itakayotoa matokeo chanya”.

TULEE VIJANA KATIKA MISINGI YA HAKI, UPENDO NA KUPENDA KAZI- DC MTAMBULE

Image
Jamii, walezi na wazazi nchini Tanzania wametakiwa kuhakikisha wanawalea watoto katika misingi ya upendo, amani, kufanya kazi na kuhakikisha wanakuwa na mchango katika Taifa kama sehemu ya kuimarisha amani na mshikamano wa Jamii na Taifa kwa ujumla. Wito umetolewa leo Jumamosi Disemba 27, 2025 na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mkoani Dar Es Salaam Mhe. Saada Ahmed Mtambule wakati wa kongamano la kidini lililofanyika Mkoani Dar Es Salaam, likijadili kuhusu amani, ustawi na maendeleo ya Jamii na Tanzania kwa ujumla wake. "Tujiulize ni mara ngapi katika wiki, mara ngapi katika mwezi sisi waumini tumekaa Baba, Mama na Watoto tunasoma Vitabu vyetu vya dini, tukatafakari mafundisho ya Mtume wetu, mara ngapi tumekaa na Vijana na watoto wetu tukazungumza masuala yanayowahusu wao na Taifa kwa ujumla na familia juu ya kuimarisha upendo, amani, kufanya kazi na kuwa na mchango kwenye Taifa letu? Tukiweza kufanya haya amani na upendo utakuwepo na matukio mengine ya rushwa na uhalifu utaweza kupun...

FAMILIA NI MSINGI WA HAKI NA USTAWI, TUZILINDE- MHE. MTAMBULE

Image
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mkoani Dar Es Salaam Mhe. Saad Ahmed Mtambule amesisitiza Waislamu na Watanzania wote kwa Ujumla kurejea katika misingi na maadili ya Kitanzania kwa kuimarisha familia na kulea Vijana katika maadili na utamaduni wa Kitanzania. Mhe. Mrambule amebainisha hayo leo Jumamosi Disemba 27, 2025 wakati wa kongamano la dini Jijini Dar Es Salaam, akisisitiza kuwa familia ndiyo msingi wa haki na ustawi wa watu na Taifa kwa ujumla, hivyo ni muhimu kuwekeza katika familia na maadili ya Mtanzania katika kukuza jamii. "Chakula kikuu cha amani ni sisi binadamu na sisi chimbuko letu si chama cha siasa ama ofisi fulani. Chimbuko letu sisi ni Familia kama Taasisi ya kwanza ya binadamu. Familia ni msingi wa amani, msingi wa haki na msingi wa ustawi wa Taifa lolote lile."Amesema Mhe. Mtambule. Katika hatua nyingine, Mhe. Mtambule amebainisha kuwa ikiwa ataonekana mtu asiyefuata maadili, mwenye kuendekeza vitendo vya rushwa, ubadhirifu na kutowajibika vyema ni kushindwa...

BAADHI YA WAUMINI WAKATOLIKI WAPINGA MAHUBIRI YA RUWA’ICHI

Image
*WASEMA KANISA SIO MTU MMOJA Na Mwandishi Wetu Baadhi ya Waumini wa Kanisa Katoliki Mkoa wa Dae es Salaam kupinga kauli za Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam Jude Thaddeus Rawai'chi ya kusema lofa”, “mpumbavu”, “njaa njaa”, “msaliti” kwa kutumia madhabahu haikuwa sawa. Waumini wamesema kuwa kama waumini waliopeleka Barua kwa ubalozi wa Vatiican kulikuwa hakuna sababu ya kutumia madhabahu badala yake wangeitwa faragha kutokana maandiko yalivyotaka. Wakizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam Waumini, Mackdeo Shilinde na Gerald Abel wamesema kauli ya Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Jude Thaddaeus k Ruwa’ichi kugeuza mimbari kuwa jukwaa la hukumu na vitisho haikuwa sawa na badala yake alitakiwa kuinjilisha Injili ya mapendo na umoja. Katika tamko lao, waumini hao wamesema kuwa kupitia kauli zake wanataka Askofu Kanisa kuendeshwe kwa misingi na inapotokea changamoto kwa waumini basi kuwepo na utatuzi unaokwenda kujenga na sio kugombana kwa kwa kutumi...

AMANI NA UTULIVU VYATAWALA SIKUKUU YA KRIMASI DAR ES SALAAM

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Maelfu ya Wananchi wa Mkoa wa Dar Es Salaam wameendelea kujitokeza katika maeneo mbalimbali Jijini hapa kwaajili ya kusherehekea Sikukuu ya Krismasi, iliyo maarufu zaidi kwa waumini wa dini ya Kiikristo kote ulimwenguni ikiwa leo ni siku ya pili maarufu kama Boxing day, siku maalum kwaajili ya kupeana zawadi za Krismasi. Suala la amani, utulivu na usalama limeshuhudiwa pia katika maeneo yenye misururu ya watu ikiwemo kwenye Fukwe za Coco (Coco Beach), Wilayani Kinondoni pamoja na eneo maarufu la Mlimani city. Katika fukwe hizo, Polisi wameonekana wakfanya doria za mguu, farasi pamoja na magari ili kuhakikisha kila mmoja anasherehekea sikukuu hiyo kwa amani na utulivu, wananchi wakiipongeza serikali na polisi kwa kuhakikisha amani inaendelea kuwepo. Kwa nyakati tofauti mara baada ya kushindwa kwa upangaji, uratibu na ufanyikaji wa maandamano yaliyokuwa haramu hapo Disemba 09, 2025, baadhi ya wanaharakati walikuwa wakihamasisha maandamano hayo kufanyika ...

RC CHALAMILA ASHIRIKI IBADA YA SIKUKUU YA CHRISTMAS USHARIKA WA KKKT KIMARA KOROGWE

Image
-Achangia ushirika wa KKKT Kimara Sadaka milioni 50. -Asema Rais Dkt Samia anatuelekeza nyakati zote kufanya kazi kwa karibu na viongozi wa Dini -Akubali mtoto mchanga aliyetoka mazingira hatarishi, anayelelewa na ushirika huo kubatizwa kwa jina lake -Asema Shauku ya Mhe Rais Dkt Samia ni kuona Kila mtanzania anafanya vitu kwa Uhuru " Amani ikitoweka Vitu vingi hutoweka. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila leo Disemba 25,2025 ameshiriki ibada ya Sikukuu ya Christmas na waumini wa usharika wa KKKT Kimara Wilaya ya Ubungo Jijini humo. Wakati wa ibada hiyo iliyongozwa na Mch. Mastai Mkuu wa Mkoa alipata wasaa wa kutoa salamu kwa waumini wa ushirika huo ambapo alisema yeye amekuja kusali hakutegemea kama angepata nafasi ya kusalimia hivyo anashukuru sana kwa kupatiwa heshima hiyo. Aidha RC Chalamila amepongeza juhudi kubwa na ubunifu unaofanywa na mchungaji Mastai wa kuendeleza ushirika huo ni dhahiri kila kitu kinaonekana wazi idadi ya waumini ni kubwa lakini pia ha...

JESHI LA POLISI LAWASHUKURU WATANZANIA KWA KUDUMISHA AMANI SIKU YA KRISMASI

Image
Na Mwandishi wetu,Dodoma Jeshi la Polisi Tanzania limetoa shukrani kwa wananchi wote nchini kwa ushirikiano waliouonyesha katika kulinda na kudumisha amani kipindi chote cha Sikukuu ya Krismasi, iliyoadhimishwa 25 Desemba 2025.  Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi Makao Makuu, Dodoma DCP David Misime ,amesema hatua hiyo imewezesha sherehe za mwaka huu kufanyika kwa utulivu na bila changamoto za kiusalama.  Amesema hali ya usalama imeendelea kuwa shwari katika maeneo yote ya nchi, huku wananchi wakiendelea kusherehekea sikukuu kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni za nchi bila wasiwasi wala hofu.  " Jeshi la Polisi limeeleza kuwa ushirikiano baina ya wananchi na vyombo vya ulinzi umekuwa nguzo muhimu katika kufanikisha dhamira ya kulinda amani na kutengeneza mazingira mazuri ya kusherehekea, "amesema Akitoa wito kwa umma, Msemaji wa Jeshi hilo amewataka Watanzania kuendelea kuilinda amani kama msingi wa maendeleo ya taifa.  “Tunaendelea...

SIMBACHAWENE AMEITAHADHARISHA JAMII YA WATANZANIA KUJIEPUSHA NA MSUKUMO WA DHULMA, UONGO NA UBINAFSI UNAOENEZWA MITANDAO YA KIJAMII

Image
  Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene ameitahadharisha jamii ya watanzania kujiepusha na msukumo wa dhulma,uongo na ubinafsi unaoenezwa kupitia mitandao ya kijamii…. … Ametoa rai hiyo leo, wakati wa Ibada ya Krismasi iliyosaliwa katika Kanisa la Parokia ya Pwaga, wilayani Mpwapwa, mkoani Dodoma huku Paroko wa Parokia hiyo,Padri Daniel Kijaji akimuombea hekima na busara katika jukumu alilokabidhiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia Suluhu Hassan la kuiongoza wizara hiyo ambapo pia alimshukuru kwa kuchangia kiasi cha Shilingi Milioni Kumi kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa hilo.

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

RUSHWA YATAJWA KUHARIBU MFUMO WA UTOAJI HAKI

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Rushwa imetajwa kuwa ni janga kubwa linaloharibu kwa kiwan go kikubwa mfumo mzima wa utoaji haki, hivyo kuhatarisha misingi ya haki, uwajibikaji na utawala bora. Kauli hiyo imetolewa leo Desemba 23, 2025 na Kamishna Msaidizi anayeshughulikia Masuala ya Ushirikishwaji wa Watanzania katika Uchumi wa Madini na Uwajibikaji wa Kampuni kwa Jamii (Local content & CSR), Terrence Ngole, ambaye amemwakirisha Katibu Mkuu Wizara ya Madini wakati akifungua mafunzo maalumu kwa Menejimenti ya Wizara ya Madini yanayolenga kujadili madhara ya rushwa pamoja na namna ambavyo rushwa inavyodhoofisha mfumo wa haki katika taasisi za umma. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Ngole amesema kuwa rushwa huathiri kwa kiasi kikubwa utekelezaji wa majukumu ya Serikali, hususan katika sekta nyeti kama utoaji wa haki, ambapo vitendo vya rushwa husababisha kukosekana kwa usawa, upendeleo na kupungua kwa imani ya wananchi kwa taasisi za umma. “Rushwa ni adui mkubwa wa ...

WAUMINI WAMPELEKA PADRI KITIMA VATIKANI, WAOMBA UCHUNGUZI WA MWENENDO WAKE

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Dar es Salaam, 22 Desemba 2025. Waumini wa Kanisa Katoliki nchini Tanzania, Stanslaus Thobias Nyakunga na Elia Phaustine Kabote, wamewasilisha rasmi barua kwa Archbishop Angelo Accattino, Balozi wa Vatican nchini, wakiomba kufanyika kwa uchunguzi wa kichungaji na kiutawala kuhusu mwenendo wa Padri Dkt. Charles Kitima, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC). Kwa mujibu wa waumini hao, hatua hiyo imechukuliwa kufuatia malalamiko na mitazamo iliyoenea kwa muda mrefu katika jamii, kwamba Padri Kitima amekuwa akihusishwa na masuala ya siasa za CHADEMA, hususan kuonekana kuingilia au kushiriki katika migogoro ya ndani ya chama hicho—jambo ambalo, wanasema, halijaonekana kwa vyama vingine vya siasa. Waumini hao wanasema mitazamo hiyo, iwe ni ya kweli au la, imeanza kuibua sintofahamu miongoni mwa waumini na kuliweka Kanisa katika mazingira yanayoweza kutafsiriwa kama ya upendeleo wa kisiasa, hali inayohatarisha nafasi ya Kanisa kama taasisi ya amani...

NAIBU WAZIRI MAKONDA AWAPA MORALI TAIFA STARS

Image
Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Christian Makonda, ametoa hamasa na morali kwa wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) pamoja na benchi la ufundi, alipokutana nao katika hoteli ya Barcelo Convention Center, jijini Fes, Morocco, ambako timu hiyo imeweka kambi ya maandalizi. Akizungumza na wachezaji na benchi la ufundi, Mhe. Makonda aliwasisitiza wachezaji kupambana kwa moyo wote, nidhamu na uzalendo wanapoivaa jezi ya Taifa, akibainisha kuwa Watanzania wote wako nyuma yao kwa kuwaunga mkono, kuwashangilia na kuwaombea ili waweze kuliletea Taifa heshima. “Taifa zima lina imani kubwa nanyi. Chezeni kwa moyo, kwa umoja na kwa kujituma, mkijua mna mamilioni ya Watanzania wanaowaombea na kuwaunga mkono,” alisema Mhe. Makonda. Katika ziara hiyo, Naibu Waziri aliambatana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw. Methusela Ntonda, Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa wizara hiyo, Bw. Abel ...