Posts

Showing posts from July, 2025

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

NCAA YANOGESHA “WORLD RANGERS DAY” KWA KUFANYA MICHEZO NA SHUGHULI ZA KIJAMII KARATU

Image
Na Philomena Mbirika, Karatu Arusha. Mamlaka ya hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) imehitimisha maadhimisho ya siku ya askari Wanyamapori duniani kwa kufanya michezo mbalimbali iliyohususu askari wa Jeshi la Uhifadhi, askari wa Jeshi la polisi wilaya ya Karatu pamoja na kufanya shughuli ya upandaji miti katika shule ya Sekondari Welwel iliyopo Karatu Mkoani Arusha. Kamishna wa Uhifadhi NCAA ameongoza maafisa na askari katika zoezi la kupanda miti Shule ya Sekondari Welweli, kutoa elimu ya shughuli za uhifadhi na utunzaji wa mazingira kwa wanananchi na kuongoza watumishi hao katika michezo mbalimbali ikiwemo kukimbia kilomita tano, mchezo wa mpira wa miguu kati ya askari wa jeshi la Uhifadhi kutoka pori lla akiba Pololeti, askari walioko eneo la hifadhi ya Ngorongoro pamoja na Polisi Karatu. “NCAA ni sehemu ya Jamii, katika utekelezaji wa majukumu yetu tunashirikiana na vyombo vingine ikiwepo Polisi Wilaya za Ngorongoro na karatu pamoja na wananchi, ndio maana leo tumefanya michezo ya...

DKT. YONAZI AWAASA WATUMISHI OFISI YA WAZIRI MKUU KUONGEZA BIDII KATIKA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO.

Image
NA.MWANDISHI WETU - DODOMA Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amewaasa Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kuendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi mkubwa katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku. Ameyasema hayo Tarehe 29 Julai, 2025 wakati akifungua Mkutano na Watumishi wa Ofisi hiyo ambapo alisema kuwa ni muhimu kuwa na nidhamu ya kazi, kushirikiana na kuendelea kuwa wabunifu katika majukumu ya kila siku, na kuwakumbusha watumishi kuwa kazi wanazofanya zinagusa maisha ya mamilioni ya wananchi, hivyo ni wajibu wa kila mtumishi kuhakikisha anatoa huduma bora na kwa viwango vya juu.  “Pia, nawasihi kuendelea kujenga mshikamano miongoni mwenu. Tunaposhirikiana, tunajenga nguvu ya pamoja ambayo hakuna changamoto inayoweza kutuzuia. Nawaomba tuendelee kufanya kazi kwa bidii na kwa moyo mmoja. Kumbukeni kuwa, kila mchango wenu una thamani kubwa katika kufanikisha malengo ya Ofisi yetu na Taifa kwa ujumla.” Alifafanua Dkt. Yonazi. Katibu Mkuu Yona...

PROF. MWANDOSYA KINARA WA MATIBABU YA SARATANI NCHINI - DKT. BITEKO

Image
*📌Dkt. Biteko azindua Kitabu cha Living with Cancer cha Prof. Mark Mwandosya* *📌 Watanzania watakiwa kujenga utamaduni wa kupima afya* *📌Serikali yaimarisha huduma za uchunguzi na matibabu ya saratani* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amemuelezea Prof. Mark Mwandosya kuwa ni Shujaa wa Saratani ya Damu (Multiple Myeloma) ambaye ameishi na Saratani kwa zaidi ya miaka 14. Dkt. Biteko amesema hayo (Julai 29) jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa kitabu cha Maisha ya Mgonjwa anayeishi na Saratani ya Damu Multiple Myeloma (Living with Cancer: Diaries of Multiple Myeloma Patient) kilichoandikwa na Prof. Mark Mwandosya ambaye ni msomi, mwandishi na mwanasiasa wa muda mrefu nchini. "Katika miaka 14 ya kishujaa, Prof. Mwandosya amekuwa shuhuda kwetu sote kuwa endapo utafuata hatua stahiki za matibabu, unaweza kupona saratani na kuendelea kuishi maisha bora. Asante sana na hongera sana Profesa. Mwenyezi Mu...

"NIKO TAYARI KUITUMIKIA UKONGA"RAGI SAMWEL

Image
      Ukonga, Dar es Salaam – Ragi Samwel, mgombea ubunge wa Jimbo la Ukonga, ameendelea kuteka hisia za wananchi kwa kujitosa katika kinyang'anyiro cha ubunge akiwa na dhamira ya kuboresha maisha ya wakazi wa jimbo hilo kupitia miradi ya maendeleo ya kiuchumi na miundombinu. ‎ ‎Ragi ameeleza kuwa ni wakati wa kuleta mabadiliko katika jimbo hilo, ambalo limekuwa na changamoto nyingi za kijamii na kiuchumi kwa muda mrefu. ‎ ‎Kwa upande mwingine, mgombea huyo alieleza kwamba changamoto za usafiri na miundombinu katika Ukonga ni miongoni mwa masuala ambayo anataka kuyaweka wazi na kuyatatua kwa ushirikiano na serikali. "Tutahakikisha kuna barabara za kisasa, usafiri wa uhakika na pia mazingira bora ya kujifunzia kwa wanafunzi wetu," alieleza. ‎ ‎Ragi alieleza pia kuwa, ili kuhakikisha mafanikio haya yanapatikana, ni lazima kuwepo na ushirikiano wa karibu kati ya viongozi wa kisiasa, wananchi na wadau mbalimbali. "Nitakuwa kiongozi wa kuungana na wananchi, kusikiliza cha...

KAMATI KUU YA CCM YARIDHIA PETER MASHILI KUVAANA NA BASHE JIMBO LA NZEGA MJINI

Image
Kamati kuu ya Chama cha Mapinduzi Taifa imempitisha Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya MASHILI COMPANY LIMITED ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mradi wa Uchenjuaji Dhahabu wa (Matinje Mining, Msilale Mining na Igurubi Mining) Ndg Peter Andrea Mashili kugombea Ubunge wa Jimbo la Nzega katika mchakato wa ndani ya chama. Mashili anachuana na wagombea 6 akiwemo Ndugu Hussein Mohamed BASHE, Regina Maganga NICHOLAUS, James Peter MALOGOTO, Dr. Francis John KIFUTUMO na Eng. Bahati Ntengo NDILLO. Mashili amabaye hivi karibuni alichukua fomu ya kuwania nafasi hiyo ya Ubunge Nzega mjini alisema kuwa ameamua Kugombea Ubunge kwa sababu wananchi wa Nzega wanahitaji nguvu na kasi Mpya ili kuendeleza utekelezaji wa ilani ya CCM katika kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka 2025-2030. Alisisitiza kuwa atajikita zaidi katika ushirikishwaji wa wananchi kwenye mambo ya msingi ya maendeleo endelevu, kuwasemea wananchi Changamoto zinaowakabili, kuwapambania ili wanufaike na Fursa zinazotolewa na Serikali...

TUNAWEZA KUZUIA ASILIMIA 80 YA VIFO NCHINI TUKIBADILI MTINDO WA MAISHA-DKT.BITEKO

Image
📌 *Asisitiza kuhusu mazoezi ya mwili ili kujikinga na maradhi yasiyoambukiza* 📌 *Apongeza NBC Dodoma Marathon kuiunga mkono Serikali mapambano dhidi ya Saratani ya Shingo ya kizazi na kusomesha Wataalam wa Afya* 📌 *Apongeza Kampeni ya MTU NI AFYA inayohamasisha Watanzania kufanya mazoezi* 📌 *NBC Dodoma Marathon yawezesha matibabu ya Saratani ya Shingo ya Kizazi kwa Wanawake 4800; mafunzo kwa Wakunga 100 na kuchangia ujenzi wa wodi* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa asilimia 80 ya vifo nchini vinaweza kuzuilika endapo Watanzania wataamua kubadili mtindo wa maisha ikiwemo kuwa na utaratibu wa kufanya mazoezi ya mara kwa mara.   Amesema hayo tarehe 27 Julai, 2025 jijini Dodoma wakati akimwakilisha Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa katika kilele cha msimu wa Sita wa NBC Dodoma Marathon 2025 ambayo imelenga kukusanya fedha kwa ajili ya kuokoa afya ya mama na mtoto. “Taarifa ya Shirika la Af...

MGOMBEA UBUNGE SIKONGE AKUMBWA NA SKENDO NZITO

Image
Wakati vuguvugu la mchujo wa wagombea ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) likizidi kupamba moto, mgombea ubunge wa Jimbo la Sikonge, Samwel Mchele Chitalilo, amejikuta katika hali ngumu baada ya kufichuliwa kwa tuhuma nzito kuhusu mienendo yake, zilizotolewa na watu wa karibu. Akizungumza na mwandishi wetu, mmoja wa watu wa karibu wa Chitalilo—ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe—alisema kuwa moja ya makosa makubwa ambayo wananchi wa Sikonge wanaweza kufanya ni kumpitisha Chitalilo kuwa mbunge, kwani hana sifa wala maadili yanayostahili kiongozi wa umma. “Huyu jamaa msimuone tu anavyotabasamu; sisi tuliomzoea tunamjua vizuri. Nimeamua kusema ukweli kwa sababu dhamira yangu hainiruhusu kunyamaza. Chitalilo ana tabia nyingi zisizofaa, ikiwemo kuchukua wake za watu bila haya, eti kwa sababu ana pesa! Amewaumiza watu wengi sana. Na suala la utapeli bado lipo—hilo halijawahi kuisha,” alieleza. Aliongeza kuwa kipindi akiwa mbunge aliwahi kumtapeli mamilioni ya fedha mfanyabiashara mmoja aitwa...

MRADI WA SEQUIP WAJENGA SHULE 6 MPYA IRAMBA-DC MWENDA

Image
Serikali kupitia mradi wa Kuboresha Ubora wa Elimu ya Sekondari (SEQUIP) imetumia Bilioni 6.361 kujenga shule mpya sita za sekondari, shule sita zimefanyiwa ujenzi wa upanuzi wa miundombinu ya kidato cha 5 na 6, Ujenzi wa vyoo na nyumba za walimu katika Wilaya ya Iramba mkoani Singida. Akitoa taarifa ya miradi ya elimu iliyojengwa katika Wilaya ya Iramba, Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mhe Suleiman Mwenda amesema kuwa ujenzi wa shule hizo utaimarisha sekta ya elimu ikiwemo kuongeza ufaulu wa wanafunzi. Amezitaja shule hizo zilizojengwa wilayani hapo kuwa ni pamoja na Ujenzi wa shule ya sekondari -MALUGA uliogharimu shilingi Milioni 470, Ujenzi wa shule ya sekondari NDULUNGU uliogharimu shilingi milioni 470, Ujenzi wa shule ya sekondari -Mtoa darajani uliogharimu shilingi milioni 544.225. Miradi mingine mipya ni pamoja na Ujenzi wa shule ya sekondari -Makunda uliogharimu shilingi milioni 544.225, Ujenzi wa shule ya sekondari-KIZEGA uliogharimu shilingi milioni 544.225, na Ujenzi wa shule ya ...

MAHAFALI YA WAFUGAJI WA KUKU WALIOHITIMU MAFUNZO YA MRADI WA SAB INVESTMENT YAFANA UBUNGO

Image
  Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  Hafla ya mahafali ya wafugaji wa kuku waliohitimu mafunzo ya ufugaji bora imefanyika leo katika wilaya ya Ubungo, Dar es Salaam, chini ya mradi ulioandaliwa na kampuni ya SAB Investment. Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali, ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mheshimiwa Albert Msando. Katika hotuba yake, Mkuu wa Wilaya alipongeza SAB Investment kwa kuanzisha mradi wenye tija unaolenga kuwajengea wananchi uwezo wa kujitegemea kiuchumi kupitia ufugaji wa kuku. Alisema kuwa mradi huo ni mfano bora wa ubunifu wa sekta binafsi katika kusaidia juhudi za serikali kuinua kipato cha wananchi na kupunguza tatizo la ajira. “Mradi huu si tu unatoa maarifa bali unawapa washiriki mbinu za kisasa za ufugaji, usimamizi wa biashara na kuongeza tija kwenye uzalishaji. Huu ni mfano wa miradi tunayotaka kuiona katika wilaya yetu,” alisema Msando. Zaidi ya washiriki 100 walihitimu mafunzo hayo, wakikabidhiwa vyeti vyao vya kuhitimu katika...

SAMIA NETBALL CUP 2025 YAZINDULIWA RASMI: ZAWADI NONO KUMNUFAISHA MWANAMKE KUPITIA MICHEZO

Image
  Dar es Salaam, 27 Julai 2025 –  Mashindano ya mpira wa netball kwa Mkoa wa Dar es Salaam, yanayojulikana kama Samia Netball Cup 2025, yamezinduliwa rasmi leo, kwa lengo la kutoa fursa kwa wanawake na mabinti kushiriki katika michezo ya netball huku wakijenga afya zao na kujiimarisha kiuchumi. Hafla hiyo ilifanyika kwenye viwanja vya Twende Pamoja na Mama Spoti Promotion, ambapo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali na mashabiki wa michezo. ‎ ‎Akizungumza na Habari Leo, mwandaaji wa mashindano hayo na Mtendaji Mkuu wa Twende Pamoja na Mama Spoti Promotion, Kasimu Ahmad, alieleza kuwa lengo kuu la mashindano haya ni kuhakikisha wanawake wanapata nafasi ya kujitokeza na kuonesha vipaji vyao katika michezo ya netball. ‎ ‎“Kumekuwa na michezo mingi, lakini kwa sasa tumeona ni muhimu kuanzisha mashindano ya netball kwa wanawake kwani wanastahili jukwaa la kuonesha vipaji vyao. Huu ni mchango wetu katika kumuunga mkono Rais Samia kwa juhudi zake za kuinua wanawake kupitia michezo,” a...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

MRADI WA SEQUIP KUMKOMBOA MTOTO WA KIKE DAR ES SALAAM NA RUVUMA

Image
Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kupitia Mradi wa kuboresha elimu ya sekondari-SEQUIP imekamilisha ujenzi wa miundombinu mbalimbali katika shule mpya za Sekondari za wasichana Dar es salaam na Ruvuma. Pamoja na dhamira hiyo ya serikali ya kuboresha sekta ya elimu kwa kuwekeza na kufanya ujenzi na ukarabati wa miundombinu kwenye shule na vyuo, pia ikiwajengea Walimu uwezo wa kiutendaji kupitia mafunzo yanayoendelea kutolewa kupitia mradi wa kuimarisha Shule Salama za Sekondari (SEQUIP). Katika kutimiza azma ya kuboresha sekta ya elimu nchini, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia inatekeleza mradi huo wa SEQUIP kwa thamani ya Dola za Kimarekani Milioni 500 ambazo ni sawa na shilingi Bilioni 1.2 kwa kipindi cha miaka mitano. Tangu kuanza kwa mradi huo mwaka wa fedha wa 2021/2022, Serikali imejenga shule mpya za sekondari na kufanya ukarabati mkubwa wa miundombinu pamoja na kutoa mafunzo ya kujenga uwezo kwa zaidi ya walimu...

MRADI WA SEQUIP KUONGEZA KIWANGO CHA UFAULU MKOANI SINGIDA-RC DENDEGO

Image
Wananchi wametakiwa kushirikiana na serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kulimda miundombinu ya shule iliyojengwa ili kuongeza ufaulu wa wanafunzi mkoani Singida. Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Halima Dendego wakati akizungumzia tathmini na hali ya elimu leo tarehe 25 Julai 2025 ambapo amesema kuwa uongozi wa mkoa huo umejipanga kuimarisha sekta ya elimu kufuatia maboresho makubwa yanayofanywa ikiwemo ujenzi wa shule mpya. Rc Dendego amesema kuwa jumla ya shule 30 za kata zimejengwa kupitia Mradi wa kuimarisha Ubora wa Elimu ya Sekondari nchini (SEQUIP) sambamba na ujenzi wa shule mpya 1 ya wasichana ya Solya iliyopo wilayani Manyoni na Ujenzi wa shule 2 mpya za Amali ya Kitukutu iliyojengwa wilayani Iramba pamoja na Unyambwa iliyojengwa katika Manispaa ya Singida. Ameongeza kuwa baada ya ujenzi wa shule hizo mkoa wa Singida umeongeza kiwango cha ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne kutoka asilimia 87 mwaka 2021 hadi asilimia 93...

MATUKIO KATIKA PICHA KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA MASHUJAA

Image
Viongozi mbalimbali wakiwasili katika Uwanja wa Mashujaa Mtumba Dodoma kushiriki Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa, Ambapo Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan anategemewa kuwa Mgeni Rasmi.Maadhimisho hayo hufanyika Julai 25 ya kila mwaka.