Posts

KASI NDOGO YA UTEKELEZAJI MRADI WA UMEME WA CHALINZE- DODOMA YAMKASIRISHA DKT. BITEKO

Image
πŸ“Œ *Asikitishwa mradi huo aliouzindua Novemba 2024 kuwa nyuma kwa asilimia Saba* πŸ“Œ *Asema Rais Samia alitoa agizo mradi usichezewe kutokana na umuhimu wake katika mikoa mbalimbali ikiwemo ya Magharibi* πŸ“Œ *Asema sababu zilizotolewa na mkandarasi (TBEA) za kusuasua kwa mradi hazikubaliki* πŸ“Œ *Atoa maagizo kwa Mkandarasi kuwasilisha mpango kazi mpya kwa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati ili kufidia muda uliopotezwa* πŸ“Œ;*Aagiza TANESCO kutumia mapato ya ndani kulipa fidia wananchi wanaopisha mradi* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekagua mradi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovolti 400 kutoka Chalinze hadi Zuzu Dodoma na kueleza kutoridhishwa kwake na utekelezaji wa mradi huo ambao ulipaswa kuwa umefikia asilimia 31 lakini kwa sasa umefikia asilimia 24 tangu kuzinduliwa kwake Novemba mwaka 2024.  Hali ya kusuasua kwa mradi imebainika wakati Dkt. Biteko akikagua mradi huo katika Kijiji cha Manchali wilayani Chamwino mkoani Dodoma tarehe 2...

TIMU YA WATAALAMU KUTOKA SADC WATEMBELEA TMA KUKAGUA NA KUKABIDHI VIFAA VYA HALI YA HEWA

Image
Dar Es Salaam; Tarahe18 Agosti 2025: Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imepokea timu ya wataalamu kutoka Kituo cha Kikanda cha Huduma za Hali ya Hewa cha Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika “SADC Climate Service Centre- (SADC CSC) wanaoratibu utekelezaji wa mradi wa SADC wa kuboresha huduma za hali ya hewa kwa nchi Wanachama wa “Intra-ACP Climate Services and related Applications (ClimSA)”.  Wataalamu hao wamefanya ziara hiyo tarehe 18 Agosti 2025 katika ofisi za TMA zilizopo Ubungo Plaza, Dar es Salaam wakiongozwa na msimamizi wa mradi huo Bi. Surekha Ramessur. Lengo kuu la ziara hiyo lilikuwa ni kukagua utendaji kazi wa vifaa ambavyo vimetolewa msaada na kituo hicho cha “SADC CSC” kwa Tanzania kupitia TMA kupitia mradi wa SADC ClimSA, na kuvikabidhi rasmi kwa TMA kwa matumizi ya kitaasisi.  Vifaa hivyo vilivyokaguliwa na kukabidhiwa kwa TMA ni pamoja na: Mtambo wa kuchakata data na kuandaa taarifa za tahadhari ya hali mbaya ya hewa (Client Workstations for ClimSA ...

MASAUNI AJIVUNIA MAENDELEO JIMBO LA KIKWAJUNI KWA MIAKA MITANO

Image
Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni, Zanzibar na mtia nia wa ubunge jimbo hilo kupitia Chama Cha Mapinduzi - CCM, Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amemshukuru Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Mwinyi kwa utekelezaji mkubwa wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020, suala lililowezesha Jimbo la Kikwajuni na Tanzania kwa ujumla kupiga hatua kubwa za Kimaendeleo. Mhe. Masauni amebainisha hayo Agosti 19, 2025 wakati akitoa tathimini ya utekelezaji wa Ilani ya CCM kwenye Jimbo la Kikwajuni pamoja na ahadi zake mbalimbali, akijivuni kasi kubwa ya maendeleo iliyopatikana katika huduma mbalimbali za Jamii, ikiwemo Ongezeko kubwa la huduma ya Maji safi na ya uhakika kwa wananchi pamoja na Ajira kwa Vijana. "Nichukue fursa hii kuwashukuru sana Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, vilevile na Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kazi kubwa na nzuri wa...

WIZARA YA NISHATI YAJIVUNIA UTEKELEZAJI WA MIRADI SABA KATI YA 17 NCHINI*

Image
*πŸ“Œ Katibu Mkuu Nishati asema kati ya miradi hiyo saba, JNHPP imekamilika* *πŸ“Œ Asema EACOP imefikia asilimia 65 huku Serikali ya Tanzania ikichangia hisa za shilingi trilioni 1.12* *πŸ“ŒRuhudji na Rumakali tafiti zakamilika* Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba amesema kuwa katika miradi ya kimkakati inayotekelezwa nchini Wizara ya Nishati inatekeleza takribani miradi saba. Mhandisi Mramba ameyasema hayo Agosti 17, 2025 wakati wa uzinduzi wa Mpango wa Uwezeshaji wa Kiuchumi kwa Vijana (YEE) ambao unagusa maeneo yanayopitiwa na mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP). “Miradi hiyo ni mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP), Mradi wa kugeuza gesi kuwa kimiminika (LNG), Mradi wa utafutaji mafuta, Miradi ya umeme ya Rumakali na Ruhudji na utafiti wa mafuta eneo la Mnazi Bay North”, amesema Mha. Mramba. Ameeleza kuwa katika miradi hiyo saba, mradi wa bwawa la kufua umeme kwa maji wa Julius Nyerere unao...

WANUFAIKA WA BIMA WAFIKIA MILIONI 25.9 NCHINI – DKT SAQWARE ‎

Image
  Na Mwandishi Wetu JAMII HURU  IMELEZWA kwamba wanufaika wa huduma za Bima nchini wamefikia milioni 25.9 kutoka mil 14 kwa mwaka 2021, huku malengo yakiwa katika miaka 10 ijayo nusu ya watanzania wawe wanatumia huduma hiyo na asilimia 95 wawe na uelewa wa kutosha kuhusu umuhimu wa bima katika maisha yao. Kamishna wa Mamlamka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), Dkt Baghayo Saqware, amesema hayo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na Wahariri na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari katika kikao cha mpango kazi kulichoandaliwa na Msajili wa Hazina. Ongezeko hilo la watumiaji wa huduma za bima limetokana na utoaji wa elimu kwa wananchi hali iliyofanya kutambua umuhimu wake katika maisha yao ya kila siku na linaloidia kukabiliana na majanga na maradhi. Aidha ameongeza kuwa licha ya kuwepo kwa mafanikio hayo ambayo wanajivunia katika kipindi cha miaka minne ya Rais Samia Suluhu Hassan, wanajipanga kuwashughulikia watoa huduma za afya wanaowapuuza wagonjwa wanaotumia b...

REA KUSAMBAZA MAJIKO BANIFU 10,650 MKOANI PWANI

Image
*πŸ“ŒRC Kunenge aipongeza REA kwa kuhamasisha matumizi nishati safi* *πŸ“ŒMifumo ya umeme jua kuchochea upatikanaji wa umeme kwa asilimia 100 ifikapo mwaka 2030* πŸ“Pwani Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imetoa jumla ya Majiko Banifu 10,650 Mkoani Pwani ikiwa ni mwendelezo wa jitihada za Serikali za kuhakikisha kila mwananchi anatumia Nishati Safi ya kupikia nchini.  Akizungumza leo tarehe 18 Agosti, 2025 ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Meneja wa Teknolojia za Nishati kutoka REA, Mha. Michael Kyessi amesema mradi huo unalenga kuuza na kusambaza Majiko Banifu kwa bei ya ruzuku ambapo mwananchi atachangia asilimia ishirini (20%) za gharama ya jiko huku asilimia themanini (80%) zikitolewa na Serikali.  “Mwananchi wa kawaida atachangia 20% tu za gharama za jiko ambapo bei ya jiko ni 56,000 na mwananchi atagharamika kuchangia shilingi 11,200 tu baada ya ruzuku kutolewa na Serikali” amesema Mha. Kyessi.  Sambamba na hilo Mha. Kyessi amebainisha thamani ya mradi huo kwa ujumla n...

DKT.BITEKO AZINDUA MRADI UTAKAOWAKWAMUA VIJANA KIUCHUMI KATIKA MAENEO YANAYOPITIWA NA BOMBA LA MAFUTA GHAFI (EACOP)

Image
πŸ“Œ *Unahusisha kuongezea vijana ujuzi, kuboresha upatikanaji wa huduma za kifedha, na kuondoa vikwazo vya ujasiriamali na ajira binafsi* πŸ“Œ *Ataka ujuzi unaotolewa kwa vijana uende sambamba na utoaji wa mitaji* πŸ“Œ *Awaasa Vijana kuchangamkia fursa na kuwa waaminifu wanapopata nafasi*  πŸ“Œ *Wanawake 6,130, Wanaume 4,905 na Makundi maalum 1,226 kufikiwa* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko leo amezindua Mpango wa Uwezeshaji wa Kiuchumi kwa Vijana (YEE) ambao unagusa maeneo yanayopitiwa na mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) ikiwa ni jitihada zinazoendelea kufanywa na Serikali katika kuhakikisha kuwa jamii zilizo karibu na miradi zinanufaika na miradi hiyo. Akizindua mradi huo katika Kijiji cha Bukombe, wilayani Bukombe, Mkoa wa Geita tarehe 18 Agosti 2025, Dkt. Biteko amesema mradi huo wa Uwezeshaji Vijana Kiuchumi ni moja ya miradi iliyopangwa kuwezeshwa na Kampuni ya EACOP kwa kipindi cha ujenzi na baada ya ujenzi ikiwa ni sehemu ya ...