Posts

TUSIKUBALI KUCHONGANISHWA NA WACHACHE WENYE MASLAHI BINAFSI- MWIGULU

Image
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba akiwa kwenye Ziara yake ya Kikazi Mkoani Arusha, amesisitiza umuhimu wa kulinda amani kwa maendeleo na ustawi wa Watanzania, akiwataka wananchi kuamka na kuwakataa wale wote wanaowachonganisha kwa maslahi yao binafsi. Akieleza kuwafahamu baadhi ya Watanzania wanaolipwa fedha ili kuwagombanisha na kuwataka kuingia barabarani kufanya vurugu, Mhe. Nchemba ameeleza kuwa wanaohamasisha vurugu nchini wamekuwa na visingizio kadhaa vya kuwahadaa wananchi huku lengo lao likiwa ni kuwagombanisha watanzania ili kutaka kuzifaidi rasilimali za nchi. "Zimetokea vurugu, kwa aina ya vurugu zilivyotokea, kwanini hatushtuki? Wanatumia visingizio vingine lakini hapa kuna mchezo. Zimetolewa fedha wakapewa vijana na wale Vijana wakaandaa Vijana wenzao na kuwataka kufanya vurugu. Leo tujiulize wale wanaotoa hizo fedha watazirudishaje? Na kama ni maandamano, Kiongozi wake alikuwa nani? Waliandamana kutoka wapi kwenda wapi? ...

Heshima Kambi ya TBN: Veronica Mrema aingia Jopo la Mdahalo Mkutano Mkuu wa Dunia wa waandishi wa sayansi

Image
PRETORIA, AFRIKA KUSINI Kilele cha utambuzi wa uandishi wa habari za kidijitali nchini Tanzania kimethibitishwa baada ya Bi. Veronica Mrema, Mwanzilishi wa chombo cha habari cha M24 TANZANIA MEDIA na mwanachama mahiri wa Tanzania Bloggers Network (TBN), kuingia rasmi kwenye jopo la mdahalo katika Mkutano wa 13 wa Kimataifa wa Waandishi wa Habari za Sayansi (WCSJ2025) unaofanyika jijini Pretoria.  Hili si tu fahari kwa Mrema binafsi, bali ni heshima kubwa kwa TBN na tasnia nzima ya habari nchini, ikionesha kuwa kazi ya uandishi wa kidijitali inatambulika katika majukwaa makuu duniani. Mrema yuko Afrika Kusini kuhudhuria mkutano huo mkuu unaotarajiwa kudumu hadi Desemba 5, 2025, baada ya kukabidhiwa udhamini maalum wa safari (Travel Grant) na Wizara ya Sayansi, Teknolojia, na Ubunifu ya Afrika Kusini (DSTI). Udhamini huu ulikuja kama matunda ya utambuzi wa utendaji wake wa kipekee katika uandishi wa habari za kisayansi na afya, akibainishwa kuwa miongoni mwa wachache barani Afrika wa...

MZEE WA UPAKO AWATAKA WATANZANIA KUJIFUNZA KUTOKANA NA TUKIO LA OKTOBA 29, "HALIPASWI KURUDIWA TENA"

Image
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo ‘Mzee wa Upako’, ametoa wito kwa Watanzania kujifunza kutokana na tukio la Oktoba 29, akisema limeleta maumivu makubwa kwa taifa na halipaswi kurudiwa tena. Amesema tukio hilo limekuwa uzoefu mpya ambao Watanzania hawakuwahi kuupitia, akiwapa pole wakazi wa Dar es Salaam, Arusha, Songwe na Mwanza ambao amesema wameguswa sana na kilichotokea. Amesema hali hiyo imemkumbusha mazingira ya mwaka 1977/1978 wakati wa vita dhidi ya Idd Amin, akieleza kuwa tukio la Oktoba 29 lilikuwa kama “vita ya wenyewe kwa wenyewe.” Pamoja na kueleza kuwa wapo waumini wake waliopigwa risasi maeneo ya Kimara, amesema hakuna Mtanzania ambaye hajaguswa, hivyo si wakati wa kulaumiana bali kila mtu ajihoji kwa nini nchi imefika hatua hiyo huku akionya kuwa kutokujifunza kutokana na kilichotokea kunaweza kusababisha tukio jingine kubwa zaidi baada ya miaka michache ijayo. Mzee wa Upako amesema ni lazima Watanzania, wakiwemo viongozi wa dini, wazazi, viongozi ...

VIJANA TUMUUNGE MKONO RAIS SAMIA KATIKA UJENZI WA TAIFA- CHILONGOLA

Image
Bw. Joseph John Chilongola, Mkazi wa Dar Es Salaam ameeleza kufurahishwa na Uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan na jitihada mbalimbali anazozichukua katika kuupata muafaka wa Kitaifa, akiwataka wananchi kujiepusha na mikumbo na hamasa za uvunjifu wa amani zinazotolewa Mitandaoni. Chilongola ameeleza namna ambavyo Rais Samia amekuwa akiongozwa na uzalendo kwa nchi yake, suala ambalo limemfanya kuwekeza zaidi katika maendeleo ya watu ikiwemo ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya barabara tena kwa kiwango cha lami katika mikoa yote nchini. "Mfano ni hapa Msongola, Kata yetu ilikuwa na shida kubwa sana ya barabara lakini sasa kwa asilimia kubwa, barabara hizo zinaelekea kutunufaisha." Amesisitiza Mwananchi huyo. Chilongola ameeleza pia kuhusu namna ambavyo vijana wamekuwa wakitumika katika matukio ya uvunjifu wa amani, akiwasihi kujiepusha na matukio hayo na kushirikiana na serikali ya awamu ya sita katika ujenzi wa Taifa lao. Amesisitiza pia kumtomkatisha tamaa Rais Samia, akitaja...

TUNAUNGA MKONO MCHAKATO WA MARIDHIANO- ZAINAB

Image
Akinamama wajasiriamali wa Mkoa wa Dar Es Salaam wamesisitiza kuhusu umuhimu wa amani katika jamii na ustawi wa familia, wakiwataka Watanzania kuwa wavumilivu na wenye subira katika kushughulikia changamoto za Kijamii na kisiasa walizonazo. Akizungumza na waandishi wa habari kutokana na athari za matukio ya uvunjifu wa amani yaliyojitokeza siku na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, Zainabu Juma, amesema mpaka hivi sasa biashara yake imefungwa kutokana na madeni yaliyotokana na siku tano walizoshindwa kufanya biashara, akisema yupo tayari kuunga mkono mchakato wa maridhiano ili kudumisha amani ya Tanzania. "Tunaomba amani ya nchi yetu, Raia wenzetu tuwe na uvumilivu kwani angalieni sisi wa hali ya chini tulivyoathirika na mpaka leo tuna madeni tumefungiwa biashara zetu na hatujui tunalipaje. Ninapenda nchi yetu iwe na amani ili tuishi kwa amani na niseme tu tupo tayari kwa maridhiano maana tunaoumia ni sisi kuanzia ndugu zetu na familia kwa ujumla." Amesema Bi. Zainab ...

TUTUMIE VYEMA FURSA YA KUUNDWA KWA WIZARA YA VIJANA- CHINONGOLO

Image
Kutokana na kuundwa kwa Wizara ya maendeleo ya Vijana nchini chini ya serikali ya awamu ya sita, Vijana wa Kitanzania wametakiwa kuiona kuwa ni fursa muhimu ya kuwajenga kiuchumi na Kijamii, wakitakiwa kuitumia vyema Wizara hiyo katika kushughulikia changamoto na fursa zinazowakabili Watanzania. Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumapili Novemba 30, 2025, Bw. Emmanuel Ephraim Chinongolo, Mkazi wa Ilala Dar Es Salaam amemshukuru pia Rais Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wake wa kuunda Wizara hiyo pamoja na kumteua Mhe. Joel Nanauka kuwa Waziri wa Wizara hiyo, akisema anaamini kuwa Wizara hiyo italeta matokeo na tija ya haraka kwa Vijana. "Ninaomba sisi Vijana tuione kama ni fursa na tuweze kujitambua kwani tukiwa wenye kujitambua itatusaidia kujua thamani ya Kijana kwenye Taifa hili na tunapaswa kujua ni wakati upi wa kupambania Taifa katika kudai amani na haki kwa njia sahihi na zisizoathiri amani yetu." Amesema Chinongolo. Aidha amesisitiza pia umuhimu wa kuilinda amani n...

REA IMEFANYA KAZI KUBWA YA KUFIKISHA HUDUMA ZA NISHATI VIJIJINI - WAZIRI NDEJEMBI*

Image
*📌Asisitiza ubunifu katika utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia* *📌Mradi wa vitongozi 9,000 mbioni kuanza* 📍Dodoma Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi ameipongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA), kwa kufikisha umeme kwenye vijiji na maeneo ya pembezoni mwa miji iliyopelekea kukuza shughuli za kiuchumi katika maeneo hayo. Pongezi hizo zimetolewa leo Novemba 28, 2025 wakati Mhe. Ndejembi alipokutana na kuzungumza na Bodi ya Nishati Vijijini (REB) pamoja na Menejimenti ya REA kuhusu utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini na vitongojini pamoja na utekelezaji wa Mkakati wa nishati safi ya kupikia katika kikao kilichofanyika Ofisi za Makao Makuu ya REA jijini Dodoma.  "REA imefanya kazi kubwa na nzuri sana hapa nchini hususan katika maeneo ya vijijini na pembezoni mwa miji. Kipekee nachukua fursa hii kuipongeza sana Bodi ya REA, Menejimenti na Wafanyakazi kwa ujumla kwa kufanya kazi kubwa ya kupeleka umeme katika vijijini vyote nchini, " Amesema Mhe. Ndeje...