Posts

BODI YA TMA YAFANYA ZIARA YA KIKAZI RADA YA HALI YA HEWA BANGULO, PUGU NA KITUO CHA HALI YA HEWA JNIA

Image
  Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imefanya ziara ya kikazi ya kukagua utendaji kazi wa Mamlaka katika kituo cha Rada ya Hali ya Hewa, Bangulo, Pugu na Ofisi za TMA zilizopo katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Dar es Salaam, tarehe 23 Julai 2025. Ziara hiyo iliongozwa na Mwenyekiti wa Bodi Mhe. Jaji Mshibe Ali Bakari na Makamu Mwenyekiti, Dkt. Emmanuel Mpeta.Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Jaji Mshibe alisema lengo la ziara ni kukagua na kutathmini usimamzi na utendaji kazi wa miundombinu ya TMA na kutathmini utekelezaji wa Maagizo na Maelekezo ya Bodi katika kuboresha huduma na pia kutambua changamoto zilizopo, na kuona Taasisi ilipo na inapoelekea. “Bodi imekuwa ikitoa maelekezo hivyo leo ilikuwa ni siku maalum kuangalia utekelezaji wake”.Alisema Jaji Mshibe. Alisisitiza kuwa TMA ya sasa imepiga hatua kubwa katika uboreshaji wa miundombinu ya utoaji huduma. Aidha, aliishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kuiwezesha Mamlaka kwa...

UTABIRI WA HALI YA HEWA KWA SAA 24 ZIJAZO

Image
 

DKT. BITEKO ATOA WITO VYOMBO VYA HABARI KUELIMISHA JAMII KUHUSU MASHUJAA

Image
📌Rais Samia mgeni rasmi Maadhimisho ya Mashujaa kesho 📌Atoa wito kwa wananchi kushiriki Maadhimisho ya Mashuja Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametoa wito kwa vyombo vya habari kushirikiana na Serikali katika kuelimisha jamii kuhusu historia ya mashujaa nchini. Dkt. Biteko ametoa wito huo Julai 24, 2025 katika Uwanja na Mnara wa Mashujaa uliopo Mji wa Serikali, Mtumba jijini Dodoma mara baada ya kukagua maadalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa. “ Ninatoa wito kwa wananchi wote kushiriki kwa wingi kwenye tukio hili adhimu. Hii ni siku yetu sote, siku ya kumkumbuka Mtanzania mwenzetu aliyesimama kwa ajili ya Taifa. Vivyo hivyo, nawaomba nyinyi waandishi wa habari, pamoja na vyombo vyenu na pia mitandao ya kijamii mshirikiane na Serikali katika kuelimisha jamii kuhusu historia ya mashujaa wetu, thamani ya mchango wao, na sababu ya sisi kuendelea kuwakumbuka kila mwaka,” amesema Dkt. Biteko. Amezungumzia maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa na k...

IUCN YAWANOA WAANDISHI KUHUSU UCHUMI WA BULUU

Image
Na Mwandishi Wetu, Tanga MRADI wa Bahari Mali unaotekelezwa na Taasisi ya International Union for Conservation Nature (IUCN), chini ya ufadhilii wa Ubalozi wa Ireland umenufaisha zaidi ya wananchi 400 wa Mkoa wa Tanga na Kisiwa cha Pemba. Hayo yamesemwa na Meneja wa Miradi ya Uhifadhi wa Habari IUCN Tanzania, Joseph Olila wakati akizungumza na mwandishi wa habari katika mafunzo kuhusu uchumi wa buluu kwa wanachama wa Chama cha Waandishi wa habari za Mazingira (JET) yanayofanyika mkoani Tanga. Olila amesema Mradi wa Bahari Mali umelenga kusaidia shughuli za uchumi wa buluu katika wilaya Mkinga na Pangani mkoani Tanga na Mkoani na Micheweni Kisiwani Pemba. Amesema katika mradi huo ambao unatatua changamoto zilizopo kwenye uchumi wa buluu, wanaangalia eneo la uzalishaji, kupitia program ya kusaidia shughuli za kijamii kwenye baadhi ya mazao ya bahari kama mwani, majongoo habari, unenepeshaji wa kaa na ufugaji wa samaki. "Lengo la programu hii ni kuwezesha wananchi kujikwamua kweny...

RAIS SAMIA KUONGOZA WATANZANIA KUMBUKUMBU YA MASHUJAA 2025

Image
Na.Mwandishi Wetu - Dodoma Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuongoza Watanzania katika Maadhimisho ya siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa, inayotarajiwa kufanyika tarehe 25 Julai, 2025 katika Viwanja vya Mashujaa Mtumba Jijini Dodoma. Akiongea na Waandishi wa Habari Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Doto Biteko, amesema Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa ni tukio muhimu linalokumbusha dhamira, ujasiri na kujitolea kwa Watanzania waliotoa maisha yao kwa ajili ya Taifa, na ametoa wito kwa wananchi kuienzi siku hiyo kwa vitendo vya uzalendo na mshikamano wa kitaifa. Dkt. Biteko amesema kuwa maadhimisho ya Siku ya Mashujaa ni fursa ya kipekee ya kutafakari mchango wa mashujaa waliolinda na kulijenga Taifa, na kuwahimiza Watanzania kuendelea kuithamini historia hiyo. “Tunapoadhimisha Siku ya Mashujaa, tunawakumbuka wale waliopoteza maisha yao kwenye medani za vita, waliostaafu baada ya kulitumikia Taifa kwa uaminifu, na wa...

BENKI YA EQUITY NA SERIKALI KUIMARISHA SEKTA YA MIFUGO NA NGOZI NCHINI

Image
Dodoma – 24 Julai 2025 Benki ya Equity kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeanzisha mpango mahsusi wa kuimarisha sekta ya Mifugo na Ngozi nchini, kwa lengo la kuongeza thamani ya mazao ya Mifugo, kupanua masoko na kuinua maisha ya wafugaji. Akizungumza katika kikao cha wadau wa sekta ya mifugo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Edwin Mhede, alisema serikali imeitaka Benki ya Equity na Bodi yake kushirikiana na serikali kuunda timu maalum ya kitaalamu itakayosimamia uwekezaji katika sekta ya Mifugo. “Hatua hii inalenga kuboresha ufugaji na mifumo ya uzalishaji wa ngozi, kuongeza ubora na kuifanya sekta hii kuwa chanzo kikuu cha mapato kwa wafugaji,” alisema Dk. Mhede. Aliongeza pia ili kuboresha Sekta ya Mifugo nchini, hasa kupambana na Magonjwa, Serikali tayari inaendesha kampeni ya kuchanja mifugo yote nchini, ambapo mpaka sasa imechanja zaidi ya mifugo milioni 16, na zoezi hili linatarajiwa kukamilika ifikapo Oktoba mwaka huu, ili kuhakikisha mazao ya Mi...

BIL 36.596 ZA MRADI WA SEQUIP ZILIVYO INUFAISHA DODOMA KWENYE SEKTA YA ELIMU

Image
Mkoa wa Dodoma ni miongoni mwa maeneo ambayo yamepata fedha nyingi kupitia mradi wa kuimarisha ubora wa Elimu ya sekondari nchini SEQUIP ambapo umepokea zaidi ya Bilioni 36.596 Fedha hizo ambazo zimetolewa na serikali zimetumika kujenga shule mpya 41 za Sekondari ambazo miongoni mwake ni pamoja na Shule 1 ya wasichana, Shule 1 ya kanda ya Wavulana, Shule za kata 36, Shule 1 ya Amali ya Mkoa, na Shule 2 za Amali za kata. Hayo yamebainishwa na Afisa Elimu Mkoa wa Dodoma Mwl Vicent Kayombo ambapo amesema kuwa fedha hizo pia zimetumika kujenga Madarasa 77, Matundu ya Vyoo 119, Maabara 19, Mabweni 22, na Nyumba za Walimu 22. Mwl Kayombo amesema kuwa mkoa wa Dodoma umejenga shule mpya ya wasichana Manchali kwa gharama ya Shilingi Bilioni 4.450 sambamba na ujenzi wa shule mpya ya Amali ya mkoa iliyojengwa katika kijiji cha Manchali wilayani Chamwino kwa gharama ya Shilingi Bilioni 1.6 Mwl Kayombo ameishukuru serikali inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi katika m...